Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Dkt. Jasson Samson Rweikiza
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bukoba Vijijini
Primary Question
MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- Je, lini Serikali itakuja na mpango wa kuhakikisha vijana wa nchi hii wanapata ajira za kutosha?
Supplementary Question 1
MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu, lakini nimwulize Mheshimiwa Naibu Waziri, je, watakubaliana nami kwamba, kutokana na uwepo wa vijana wengi sana wasiokuwa na ajira, ni dhahiri kwamba mipango yote iliyopo haijafanikiwa kutatua tatizo hili?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Nilitoa ushauri huko nyuma kuhusu makambi ya kilimo kwa vijana. Siyo kweli kwamba kama yangetekelezwa, tatizo hili lingeisha kabisa na kuondoka katika Taifa hili?
Name
Rahma Riyadh Kisuo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA MAHUSIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tunakubaliana sote kuwa suala la changamoto la ajira siyo kwa Tanzania pekee, hili ni suala la dunia nzima. Hata hivyo, Serikali imeendelea kutekeleza program na mikakati mbalimbali kama nilivyoeleza kwenye jibu la swali la msingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi kwa mwaka 2024, kiwango cha ukosefu wa ajira nchini kimepungua kutoka 8.2% mwaka 2021 hadi 6.2% mwaka 2024. Serikali itaendelea kupanga na kutekeleza mipango na program hizo na nyingine ili kuendelea kupunguza tatizo la ajira nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali lake la pili, Serikali ilipokea ushauri wa Mheshimiwa Mbunge na moja ya utekelezaji wake ni Program ya Jenga Kesho Iliyobora ya BBT kutoka Wizara ya Kilimo ambapo vijana wanaendelea kunufaika na program hiyo. Aidha, Serikali itaendelea kuweka mikakati na kutekeleza kwa lengo la kuondoa au kupunguza tatizo la ajira nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha. (Makofi)
Name
Kunti Yusuph Majala
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- Je, lini Serikali itakuja na mpango wa kuhakikisha vijana wa nchi hii wanapata ajira za kutosha?
Supplementary Question 2
MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipatia fursa nami nipate kuuliza swali la nyongeza. Ni ukweli usiopingika kwamba, kasi ya Serikali ya uongezaji wa ajira kwa vijana haiendani na ongezeko la vijana nchini na badala yake vijana wameamua kuchagua fursa ya kujishughulisha na shughuli za usafirishaji kwa maana ya bodaboda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kutoa mikopo na vijana wale wameona njia rahisi ya mikopo wanayopewa kwa sababu haikidhi kwenye mitaji mikubwa, wanapewa fedha ndogo wameamua kwenda kununua bodaboda. Tunawapa bodaboda vijana wetu wakiwa wazima, lakini baada ya miezi, miaka tunarudi kuja kuwapa mikopo wakiwa walemavu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina mkakati gani wa kuweza kuokoa vijana wa Taifa hili kwa ajili ya kuweza kuwa na viongozi, na kupunguza gharama kubwa za kuja kuwahudumia walemavu tunaowatengeneza sisi wenyewe kama Taifa? (Makofi)
Name
Rahma Riyadh Kisuo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA MAHUSIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kama nilivyosema kwenye jibu la msingi, inaendelea kutekeleza mikakati mbalimbali katika kuwawezesha vijana kujiajiri na kupata ajira. Hivyo, suala la Mheshimiwa Mbunge, sisi tumelipokea kama Serikali na hivi karibuni tutawajia hapa hapa kuwapa mkakati mzuri tuliopanga kama Serikali kuweza kumudu madhila yanayotokea ya vijana katika shughuli zao wanazozitumia kujitafutia riziki za kila siku.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha. (Makofi)
Name
Hija Hassan Hija
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kiwani
Primary Question
MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- Je, lini Serikali itakuja na mpango wa kuhakikisha vijana wa nchi hii wanapata ajira za kutosha?
Supplementary Question 3
MHE. HIJA HASSAN HIJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba niulize swali la nyongeza. Mheshimiwa Waziri, amethibitisha kwamba vijana 6,367 wamepata ajira nje ya nchi, na vijana wengi wamekuwa na utashi wa ajira hizi, lakini wanakwazwa na masuala ya lugha. Je, Serikali ina mpango gani wa kuandaa program maalum kwa ajili ya Watanzania ili wawe na lugha nzuri ambayo inakubalika nje?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, je,...
MWENYEKITI: Mheshimiwa, swali la nyongeza ni moja tu.
MHE. HIJA HASSAN HIJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA MAHUSIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, sijasikia swali vizuri.
MWENYEKITI: Naibu Waziri, hajasikia vizuri, hebu uliza kwa ufasaha.
MHE. HIJA HASSAN HIJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni kwamba, Serikali imekiri kwamba vijana 6,367 wamepata ajira nje ya nchi. Vijana wengi wamekuwa na ari ya kufanya ajira hizo, lakini wanakwazwa na masuala ya lugha. Serikali ina mpango gani wa kuwaandaa vijana wetu ili wakidhi kigezo hicho?
Name
Rahma Riyadh Kisuo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA MAHUSIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, tunatoa mafunzo maalum mahususi kwa vijana wanaokwenda nje kwa ajili ya kufanya kazi. Naomba tupokee ushauri wa Mheshimiwa Mbunge, juu ya mafunzo ya lugha, tuongeze katika program yetu ya mafunzo ambayo vijana wanapewa kabla ya kwenda kufanya kazi nje ya nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha. (Makofi)
Name
Lucy Edward Mwakyembe
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- Je, lini Serikali itakuja na mpango wa kuhakikisha vijana wa nchi hii wanapata ajira za kutosha?
Supplementary Question 4
MHE. LUCY EDWARD MWAKYEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nami napenda kumwuliza Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba, nchi yetu tunajua inakwenda kwenye ajenda ya fifty fifty katika uongozi. Je, wanawafikiriaje vijana wa kike katika kuwapa kipaumbele katika ajira?
Name
Rahma Riyadh Kisuo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA MAHUSIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikalini hatutoi ajira kwa upendeleo, kwa maana ya kwamba sheria inasema tutatoa ajira bila kujali jinsia, rangi, wala kabila. Tutatoa ajira kwa usawa. Kwa hiyo, kuelekea Dira ya 2050 Serikali itaendeleza jitihada zake za kutoa ajira kwa usawa bila kujali jinsia ili kutekeleza Dira hiyo ya 2050.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved