Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Silvery Luboja Salvatory

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Primary Question

MHE. SILVERY L. SALVATORY aliuliza:- Je, lini Serikali itamrejesha mkandarasi wa ujenzi wa Barabara ya Mwanangwa – Misasi – Salawe – Kahama kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. SILVERY L. SALVATORY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza ninakubaliana na mpango wa Serikali wa kutengeneza barabara kwa awamu kwa sababu za kibajeti, lakini majibu ya Mheshimiwa Waziri ni tofauti kabisa na hali halisi iliyoko site kwa kuwa Serikali haijasema kweli. Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuambatana na mimi kwenda kujionea hizo 40% za ujenzi wa kilometa tatu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Ninaomba Serikali sasa iwaambie wananchi wa Mwanangwa, Misasi, Buhingo, Busongo, na Nunduru, ni lini barabara yao itaanza kujengwa kiukweli? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba mkandarasi alishafanya kazi na ndiyo maana alishaomba hata malipo baada ya kufanya kazi. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tulichoandika hapa, niko tayari kwenda na Mheshimiwa Mbunge kuona kile ambacho kimefanyika, lakini huku Serikali ikiwa inaandaa malipo ya huyo mkandarasi ili aweze kuendelea na kazi.

Mheshimiwa Spika, pia nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni dhamira ya Serikali na ndiyo maana tumeanza kuijenga kwa awamu tukisubiri kupata fedha nyingi ambayo tutakamilisha kuijenga barabara hiyo ya Misungwi mpaka Kahama.

Mheshimiwa Spika, tusingekuwa na dhamira ya dhati tusingeanza, lakini tumeona wakati tunapata fedha kiasi, basi tuendelee kupunguza kazi, lakini tutakapokuwa tumepata fedha yote, mpango wa Serikali ni kujenga barabara yote kutoka Misungwi hadi Kahama kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Zacharia Paulo Issaay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. SILVERY L. SALVATORY aliuliza:- Je, lini Serikali itamrejesha mkandarasi wa ujenzi wa Barabara ya Mwanangwa – Misasi – Salawe – Kahama kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana. Ninaishukuru sana Serikali kwa kazi kubwa na kumlipa mkandarasi wa barabara ya Mbulu - Garbabi - Haydom. Je, kwa kuwa mkandarasi huyu hadi sasa hajarudi site, ni lini mkandarasi wa Mbulu - Garbabi - Haydom atarudi na kuanza kufanya kazi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, ni kweli tuna vipande viwili Mbulu - Garbabi na Labay - Haydom ambapo mkandarasi anayetekeleza ni mkandarasi mmoja na tumeshamlipa fedha aliyokuwa anatudai. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mkandarasi atarudi site kwanza kufanya kazi ya kuhakikisha kwamba zile njia za diversion zinapitika, lakini pia kuendelea na kazi ya ujenzi kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kumwagiza Meneja wa Manyara ahakikishe mkandarasi anarudi site na kuhakikisha kwamba maeneo yote ambayo yalikuwa na changamoto za kutopitika yanapitika wakati anaanza kuijenga hiyo barabara yote kwa kiwango cha lami katika vipande hivyo viwili.