Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 13 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 153 | 2026-04-21 |
Name
Silvery Luboja Salvatory
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Misungwi
Primary Question
MHE. SILVERY L. SALVATORY aliuliza:-
Je, lini Serikali itamrejesha mkandarasi wa ujenzi wa Barabara ya Mwanangwa – Misasi – Salawe – Kahama kwa kiwango cha lami?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Silvery Luboja Salvatory, Mbunge wa Misungwi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Mwanangwa – Misasi – Salawe – Kahama yenye urefu wa kilometa 149 unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha kwa kuanza na sehemu ya Mwanangwa hadi Manawa kilometa tatu ambapo utekelezaji wake umefika 40%. Kwa sasa, Serikali inaendelea na taratibu za kupata fedha ili kumlipa mkandarasi madai yake aweze kuendelea na kazi, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved