Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 13 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 153 2026-04-21

Name

Silvery Luboja Salvatory

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Primary Question

MHE. SILVERY L. SALVATORY aliuliza:-

Je, lini Serikali itamrejesha mkandarasi wa ujenzi wa Barabara ya Mwanangwa – Misasi – Salawe – Kahama kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Silvery Luboja Salvatory, Mbunge wa Misungwi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Mwanangwa – Misasi – Salawe – Kahama yenye urefu wa kilometa 149 unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha kwa kuanza na sehemu ya Mwanangwa hadi Manawa kilometa tatu ambapo utekelezaji wake umefika 40%. Kwa sasa, Serikali inaendelea na taratibu za kupata fedha ili kumlipa mkandarasi madai yake aweze kuendelea na kazi, ahsante.