Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Charles Mhando Njama
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Korogwe Mjini
Primary Question
MHE. CHARLES M. NJAMA aliuliza:- Je, Serikali haioni kuwa ipo haja ya kujenga majengo mapya katika Hospitali ya Magunga badala ya kuendelea kuweka viraka kila mwaka?
Supplementary Question 1
MHE. CHARLES M. NJAMA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Ninamshukuru sana Mheshimiwa Waziri na Serikali kwa namna ambavyo wameendelea kutoa jicho lao kwa ajili ya ukarabati wa majengo yale, lakini kwa kuwa hali ya majengo yale ni chakavu mno na hayaridhishi kabisa, tunaomba aweze kupanga safari yeye pamoja na wataalam wake ili twende tukaone hali halisi kwa pamoja.
Mheshimiwa Spika, ninaamini baada ya kuiona tunaweza tukawa na mpango wa pamoja ambao utatufanya tuharakishe zaidi kufanya matengenezo, kwa kuwa kiasi cha milioni 600,000,000 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 bado ni kidogo mno ukilinganisha na hali ya uhitaji uliokuwepo katika majengo yale.
Mheshimiwa Spika, swali la pili. Je ni lini ujenzi wa kituo cha afya katika Kata ya Kwamndolwa utaanza, kwa kuwa imekuwa ahadi ya muda mrefu kwa wananchi wa Kwamndolwa? Ahsante.
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, pongezi ambazo amezitoa Mheshimiwa Mbunge zinaelekea moja kwa moja kwa Rais, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa sababu yeye alifanya ziara na aliahidi fedha hizi ziende kwa ajili ya kukamilisha miundombinu ambayo imetajwa.
Mheshimiwa Spika, ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge, baada ya Bunge lako Tukufu, tutapanga ratiba ili twende ziara katika hospitali yetu hii kujionea uchakavu wa miundobinu na pia thamani ya fedha ambayo imetengwa kwa ajili ya kukamilisha miundobinu hiyo.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishe Mheshimiwa Mbunge kwamba katika swali lake la pili la nyongeza kuhusu kituo cha afya, tukiwa katika ziara hii tutapita kwenye kituo cha afya alichokitaja ili tuone namna gani ya kuendelea kutenga fedha ili kukamilisha miundobinu ya ujenzi wa kituo hicho.
Name
Haiderali Hussein Gulamali
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ilongero
Primary Question
MHE. CHARLES M. NJAMA aliuliza:- Je, Serikali haioni kuwa ipo haja ya kujenga majengo mapya katika Hospitali ya Magunga badala ya kuendelea kuweka viraka kila mwaka?
Supplementary Question 2
MHE. HAIDERALI H. GULAMALI: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana. Ninataka kujua, ni lini Hospitali ya Manispaa ya Mpanda itapata jengo la emergency?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimejibu kwenye majibu ya awali, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Hospitali ya Mpanda nayo imo katika mpango wa zile hospitali 105 ambazo tumeshatenga bajeti katika mwaka wa fedha 2026/2027, jumla ya shilingi bilioni 52.25, ambazo tutazielekeza katika kukamilisha baadhi ya miundombinu muhimu.
Mheshimiwa Spika, ni kweli jengo la emergency ni muhimu sana kwa sababu linatoa huduma kwa wakati na baadhi ya wagonjwa huishia tu kutibiwa emergency na kwenda nyumbani. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tutaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya ujenzi wa jengo hili muhimu.
Name
Dr. George Venance Lugomela
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Maswa Mashariki
Primary Question
MHE. CHARLES M. NJAMA aliuliza:- Je, Serikali haioni kuwa ipo haja ya kujenga majengo mapya katika Hospitali ya Magunga badala ya kuendelea kuweka viraka kila mwaka?
Supplementary Question 3
MHE. DKT. GEORGE V. LUGOMELA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa tuna Kata ya Ipililo, kimejengwa kituo cha afya katika Kata ile na Kata ya Ipililo ndiyo Kata yenye wakazi wengi katika Jimbo la Maswa Mashariki. Ninaomba kuuliza, je, kituo cha afya hiki kitaanza kufanya kazi lini?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge aliuliza swali la nyongeza kuhusu kituo cha afya Kata ya Maswa. Kwanza tumejielekeza kutoa katika vile vituo ambavyo havijakamilika kwanza viweze kutoa huduma zile za OPD. Kwa hiyo, mimi na Mheshimiwa Mbunge tutakaa chini baada ya Bunge hili leo, ili tuone namna gani katika kituo chetu hiki cha afya kitaanza kutoa huduma za msingi kwa ajili ya wananchi wetu.
Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.
Name
Kija Limbu Ntemi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Katoro
Primary Question
MHE. CHARLES M. NJAMA aliuliza:- Je, Serikali haioni kuwa ipo haja ya kujenga majengo mapya katika Hospitali ya Magunga badala ya kuendelea kuweka viraka kila mwaka?
Supplementary Question 4
MHE. KIJA L. NTEMI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi hii ili na mimi niulize swali. Kituo cha Afya cha Katoro kinapokea wagonjwa wengi sana kuliko Hospitali ya Wilaya ya Katoro. Je, ni lini Kituo cha Afya cha Katoro kitapata jengo la emergence ili kuongeza ufanisi kuhudumia wananchi wa Katoro?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, ni kweli pale Katoro kuna ongezeko kubwa sana la watu ndiyo maana wananchi wetu wanaona bora waende kwanza wakapate huduma katika kituo cha afya, lakini tayari Katoro wanayo hospitali ya wilaya inayotoa huduma za msingi, na wana jengo bora kabisa la emergency.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunawaomba wananchi waendelee kwenda kupata huduma hizo katika jengo la dharura la hospitali yetu ya Wilaya huku tukiendelea kujielekeza kuboresha miundobinu rafiki na miundobinu ya dharura katika kituo chetu cha Afya cha Katoro.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved