Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 13 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 146 | 2026-04-21 |
Name
Charles Mhando Njama
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Korogwe Mjini
Primary Question
MHE. CHARLES M. NJAMA aliuliza:-
Je, Serikali haioni kuwa ipo haja ya kujenga majengo mapya katika Hospitali ya Magunga badala ya kuendelea kuweka viraka kila mwaka?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Charles Mhando Njama, Mbunge wa Korogwe Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, hospitali ya Magunga ni moja ya hospitali kongwe nchini ambayo imejengwa mwaka 1952 na inahitaji ukarabati mkubwa. Katika Mwaka wa Fedha 2025/2026 Serikali imetoa jumla shilingi bilioni 1.06 kwa ajili ya ujenzi wa jengo jumuishi la huduma za uzazi Maternity Complex kwa muundo wa ghorofa. Taratibu za kibali na michoro zinaendelea.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2026/2027, Serikali imetenga fedha shilingi milioni 600 kwa ajili ya ujenzi wa theatre pamoja na ukarabati wa jengo la kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Magunga. Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mipya inayohitajika katika Hospitali ya Magunga ili iweze kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.
Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved