Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 13 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 146 2026-04-21

Name

Charles Mhando Njama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. CHARLES M. NJAMA aliuliza:-

Je, Serikali haioni kuwa ipo haja ya kujenga majengo mapya katika Hospitali ya Magunga badala ya kuendelea kuweka viraka kila mwaka?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Charles Mhando Njama, Mbunge wa Korogwe Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, hospitali ya Magunga ni moja ya hospitali kongwe nchini ambayo imejengwa mwaka 1952 na inahitaji ukarabati mkubwa. Katika Mwaka wa Fedha 2025/2026 Serikali imetoa jumla shilingi bilioni 1.06 kwa ajili ya ujenzi wa jengo jumuishi la huduma za uzazi Maternity Complex kwa muundo wa ghorofa. Taratibu za kibali na michoro zinaendelea.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2026/2027, Serikali imetenga fedha shilingi milioni 600 kwa ajili ya ujenzi wa theatre pamoja na ukarabati wa jengo la kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Magunga. Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mipya inayohitajika katika Hospitali ya Magunga ili iweze kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.