Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Dr. Wilson Charles Mahera
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Butiama
Primary Question
MHE. DKT. WILSON C. MAHERA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa majengo muhimu yanayohitajika katika Hospitali ya Wilaya Butiama?
Supplementary Question 1
MHE. DKT. WILSON C. MAHERA: Mheshimiwa Spika, ninapenda kuchukua nafasi hii kwanza kuishukuru Serikali kwa kutenga fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa majengo saba, ambayo yanaendelea kujengwa kwa sasa. Uhakika ni kwamba, majengo ambayo yamekamilika ni manne. Sasa majengo tisa ambayo bado yanahitajika, kwa mfano jengo la huduma ya macho, jengo la kuhifadhia maiti, majengo ya huduma ya kinywa na meno, pamoja na karakana ya hospitali na jiko, haya ni majengo muhimu sana ambayo yanahitajika.
Mheshimiwa Spika, je, Serikali ina mkakati gani kuongeza kasi kuhakikisha kwamba majengo haya yanakamilika ili wananchi wa Butiama waweze kupata huduma nzuri ya afya? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili. Ninamwomba Mheshimiwa Waziri ikiwezekana mwezi wa Saba tuambatane naye aende kuangalia hali halisi ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Butiama, ahsante.
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, tunaendelea kusisitiza ukamilishaji wa majengo haya na tunawaelekeza wataalamu wetu kuwa waadilifu katika kazi hii. Tayari Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, imetuma baadhi ya timu yetu kwenda kuangalia ujenzi wa mejengo haya ili yakamilike kwa wakati.
Mheshimiwa Spika, nikijibu swali lake la pili, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, tuko tayari muda wowote kufanya ziara. Ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge, baada ya Bunge lako hili Tukufu la Bajeti tutaongozana naye kwenda Butiama kujionea miundombinu hii, ili iweze kutoa huduma kwa wananchi wetu. (Makofi)
Name
Dotto Jasson Bahemu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ngara
Primary Question
MHE. DKT. WILSON C. MAHERA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa majengo muhimu yanayohitajika katika Hospitali ya Wilaya Butiama?
Supplementary Question 2
MHE. DOTTO J. BAHEMU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Sisi Hospitali yetu ya Wilaya ya Ngara, na ya Mbuba, pia kuna ujenzi ambao unaendelea, lakini jengo la mochwari, jengo la wodi za wagonjwa pamoja na theatre vilevile bado hayajakamilika. Je, ni mpango gani wa Serikali kuhakikisha kwamba haya majengo yanakamilika ili wananchi waendelee kupata huduma bora sana. Ahsante. (Makofi)
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, sote tutakumbuka kwamba Serikali katika bajeti ya mwaka 2026/2027 tumetenga zaidi ya shilingi bilioni 52.25 kwa ajili ya ukamilishaji wa majengo, miundombinu katika hospitali zetu za Halmashauri 105. Nimhakikishie Mheshimiwa Bahemu, yupo ndani ya mpango, tutakwenda wote pamoja kuhakikisha kwamba hospitali hii tunakwenda kuikamilisha katika miundombinu hiyo.
Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.
Name
Innocent Lugha Bashungwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Karagwe
Primary Question
MHE. DKT. WILSON C. MAHERA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa majengo muhimu yanayohitajika katika Hospitali ya Wilaya Butiama?
Supplementary Question 3
MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Spika, kwanza ninaomba niishukuru Serikali kwa kupeleka fedha awamu ya kwanza kujenga Kituo cha Afya cha Tarafa ya Nyakakika. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha awamu ya pili ili kukamilisha kituo cha afya? Ahsante sana. (Makofi)
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, tayari tulishapeleka fedha awamu ya kwanza, na tayari tumeshaomba fedha Hazina awamu ya pili ili kuhakikisha tunakamilisha kwa wakati vile vituo vyote ambavyo tulivianzisha ambavyo tulivitengea shilingi milioni 250. Nimhakikishie Mheshimiwa Bashungwa, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, tutaendelea kutoa ushirikiano wa dhati kuhakikisha kituo hiki kinakamilika kwa wakati.
Name
Morris Joseph Makoi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Moshi Mjini
Primary Question
MHE. DKT. WILSON C. MAHERA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa majengo muhimu yanayohitajika katika Hospitali ya Wilaya Butiama?
Supplementary Question 4
MHE. MORRIS J. MAKOI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Ninaomba kumwuliza Naibu Waziri atusaidie, Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kukarabati kituo kikongwe cha afya cha Umbwe ambacho kipo Kibosho Magharibi, kituo ambacho kinawanahudumia Tarafa yote ya Kibosho yenye Kata sita?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, tayari tuna mpango mkakati pale Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kuhakikisha vituo vya afya kongwe, na hospitali zile kongwe tumezitengea bajeti kwa ajili ya kwenda kuzikamilisha, ikiwa ni pamoja na kurekebisha miundombinu chakavu ili ziendelee kutoa huduma kwa wakati.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa tutaendelea kutenga bajeti ili kukamilisha vituo kongwe kama ambacho amekiongelea.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved