Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 13 | Regional Administration and Local Government Authorities | Wizara ya Viwanda , Biashara na Uwekezaji | 145 | 2026-04-21 |
Name
Dr. Wilson Charles Mahera
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Butiama
Primary Question
MHE. DKT. WILSON C. MAHERA aliuliza: -
Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa majengo muhimu yanayohitajika katika Hospitali ya Wilaya Butiama?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, naomba kumjibu Mheshimiwa Dkt. Wilson Mahera, Mbunge wa Jimbo la Butiama:-
Mheshimiwa Spika, Hospitali ya Butiama ni moja kati ya hospitali 25 ambazo zimejengwa katika awamu ya tatu ya ujenzi wa hospitali za halmashauri ambao ujenzi ulianza mwaka 2021/2022. Jumla ya majengo tisa yamejengwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Butiama kwa gharama ya shilingi bilioni 3.02.
Mheshimiwa Spika, majengo yaliyokamilika ni pamoja na jengo la OPD, maabara, EMD, jengo jumuishi la uzazi, yaani martenity complex. Aidha, jengo la OPD limekamilika na huduma za wagonjwa wa nje zimeanza kutolewa mwezi Novemba, 2024.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2026/2027 hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Butiama imetengewa shilingi milioni 500, kwa ajili ya ukamilishaji wa majengo yaliyosalia. Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa awamu, kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu muhimu katika hospitali za Halmashauri Wilaya ya Butiama.
Mheshimiwa Spika, ninaomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved