Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 13 Regional Administration and Local Government Authorities Wizara ya Viwanda , Biashara na Uwekezaji 145 2026-04-21

Name

Dr. Wilson Charles Mahera

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Primary Question

MHE. DKT. WILSON C. MAHERA aliuliza: -

Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa majengo muhimu yanayohitajika katika Hospitali ya Wilaya Butiama?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, naomba kumjibu Mheshimiwa Dkt. Wilson Mahera, Mbunge wa Jimbo la Butiama:-

Mheshimiwa Spika, Hospitali ya Butiama ni moja kati ya hospitali 25 ambazo zimejengwa katika awamu ya tatu ya ujenzi wa hospitali za halmashauri ambao ujenzi ulianza mwaka 2021/2022. Jumla ya majengo tisa yamejengwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Butiama kwa gharama ya shilingi bilioni 3.02.

Mheshimiwa Spika, majengo yaliyokamilika ni pamoja na jengo la OPD, maabara, EMD, jengo jumuishi la uzazi, yaani martenity complex. Aidha, jengo la OPD limekamilika na huduma za wagonjwa wa nje zimeanza kutolewa mwezi Novemba, 2024.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2026/2027 hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Butiama imetengewa shilingi milioni 500, kwa ajili ya ukamilishaji wa majengo yaliyosalia. Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa awamu, kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu muhimu katika hospitali za Halmashauri Wilaya ya Butiama.

Mheshimiwa Spika, ninaomba kuwasilisha.