Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Onesmo Merdson Mnkondya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbozi
Primary Question
MHE. ONESMO M. MNKONDYA aliuliza: - Je, lini Serikali italipa fidia kwa Wananchi waliopisha eneo la JKT Itaka?
Supplementary Question 1
MHE. ONESMO M. MNKONDYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninaishukuru Serikali kwa majibu mazuri ambayo inaendelea kuyatoa, lakini ninaomba niwe na maswali mawili ya nyongeza kwa Waziri wangu wa Ulinzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, wananchi hawa tangu mwaka 2022 wamekuwa na uvumilivu wa hali ya juu sana 2023, 2024 hadi 2025 na leo 2026 mnawaambia waendelee kuvumilia na waendelee kuwa na subira. Hii subira ni mpaka lini watapewa fedha zao wananchi hawa ambao wana shida sana?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Wananchi hawa pia wana madai ya kwamba, ardhi yao imepanda thamani kwa sababu ya kucheleweshewa malipo yao na wengine wanadai ardhi yao warudishiwe waweze kuiendeleza na kuitumia. Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari mimi na yeye tuandae mkutano kwa ajili ya wananchi hawa, tuonanenao, tuzungumzenao, pengine awape majibu zaidi ya Serikali kwa ajili ya madai yao ya shilingi bilioni 5.7? Ahsante.
Name
Rhimo Simeon Nyansaho
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nominated
Answer
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakiri kwamba ni kweli wananchi wetu wa Itaka wamekuwa wavumilivu, lakini Serikali imelipa kipaumbele hili suala. Ndiyo maana tayari tumewasilisha fedha hizo shilingi bilioni 5.7 kwa ajili ya kuhakikisha kwamba wanalipwa na tayari tuliweka kwenye bajeti iliyopita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali, kwa maana ya Wizara yetu ya Ulinzi, inafanya mawasiliano ya karibu sana na Wizara ya Fedha ili kuhakikisha kwamba kabla mwaka wa fedha haujaisha wananchi wetu wawe tayari wameanza kulipwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, swali la pili, Mheshimiwa Mbunge ameomba niweze kuambatana naye kwa ajili ya kuzungumza na wananchi wetu wale. Niko tayari kwa ajili ya kuambatana na Mheshimiwa Mbunge, ili tuweze kutafuta suluhu ya maswali ambayo watauliza na kutoa ufafanuzi, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved