Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Dr. Christina Christopher Mnzava
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Halmashauri ya Shinyanga?
Supplementary Question 1
MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, ninapenda kumshukuru Naibu Waziri TAMISEMI kwa majibu yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali hii ya Halmashauri ya Shinyanga imeanza kujengwa mwaka 2008 mimi nikiwa mtumishi wa Halmashauri kama Medical Officer in Charge na msimamizi wa ujenzi ule. Awamu ya mwaka 2018/2019 imekuta ile hospitali tayari imeshaanza kujengwa, lakini haijakamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni upi mpango mkakati wa Serikali kutoa kipaumbele kwa Halmashauri ya Shinyanga, hizi shilingi milioni 200 zilizotengwa? Tunahitaji shilingi milioni 500 tu kukamilisha ujenzi ule. Je, ni nini mpango mkakati wa Serikali kuipa kipaumbele Halmashauri ya Shinyanga? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Ujenzi wa majengo ya kutolea huduma umekwenda sambamba na ujenzi wa nyumba za watumishi. Pale kuna nyumba tatu tu, kuna madaktari 17 ambao tunahitaji wakae eneo la hospitali. Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za watumishi? (Makofi)
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye majibu yangu ya msingi, shilingi milioni 200 hizi zinaelekezwa kwenda kukamilisha yale majengo saba yaliyosalia, lakini tutafanya tathmini kuona uhitaji na kuweza kuwaongezea bajeti kadiri tunavyopokea fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kuhusu nyumba za watumishi, nilishajibu katika Bunge lako Tukufu. Tayari tumefanya tathmini na uhitaji zaidi ya nyumba 2,000 na tunahitaji zaidi shilingi bilioni 241 ambazo tayari TAMISEMI imeshaanza kushirikiana kuzitafuta fedha hizi ili kuona namna tunavyoweza kukamilisha nyumba hizi ambazo tutazielekeza pia katika Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha.
Name
Cecilia Daniel Paresso
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Halmashauri ya Shinyanga?
Supplementary Question 2
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kazi kubwa iliyofanyika ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Karatu na huduma zinazoendelea kutolewa, bado kuna upungufu wa ukosefu wa jiko kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa. Wakati wa ziara ya Waziri Mkuu Wilayani Karatu, tuliahidiwa kwamba fedha zitaletwa. Je, ni lini fedha hizo zitaletwa ili utekelezaji na ujenzi wa jiko uweze kufanyika?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Wilaya ya Karatu ni miongoni mwa hospitali ambazo zimo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 ambapo tumetenga jumla ya shilingi bilioni 56.25 kwa ajili ya ukamilishaji wa hospitali 105.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Paresso, tutapanga bajeti kulingana na ukamilishaji wa miundombinu ambayo inapelea katika Hospitali yetu ya Karatu.
Name
Fadhili Sandali Chilombe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduru Kusini
Primary Question
MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Halmashauri ya Shinyanga?
Supplementary Question 3
MHE. ENG. FADHILI S. CHILOMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Kituo cha Afya Mtina kinachohudumia kata mbili, hakina jengo la mama na mtoto, hali inayosababisha staha ya wakina mama kuondoka hasa wakati wanapojifungua. Tulishaanzisha ujenzi pale na jengo halijakamilika, nini mpango wa Serikali kukamilisha jengo hilo? (Makofi)
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza Mheshimiwa Eng. Fadhili, Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kusini kwa kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa vituo hivi vya afya ambavyo tayari tulishaanza kujenga na tunatoa huduma zile za OPD, lakini tunajua miundombinu ambayo bado inatakiwa kukamilishwa, tunaendelea kutenga bajeti kukamilisha miundombinu hiyo.
Name
Azza Hilal Hamad
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Halmashauri ya Shinyanga?
Supplementary Question 4
MHE. AZZA H. HAMAD: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa hospitali ya Wilaya ya Halmashauri ya Shinyanga inahudumia majimbo mawili yenye kata 26 na hivyo kuwafanya wananchi wa Jimbo la Itwangi kutembea umbali mrefu kwa ajili ya kupata huduma ya Hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kukipandisha hadhi Kituo cha Afya cha Tinde ili kiwe na hadhi ya kiwilaya kutokana na mazingira yaliyopo? (Makofi)
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI, MKUU TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Azza, Mbunge wa Jimbo la Itwangi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninampongeza kwa kuendelea kufuatilia hali ya Kituo cha Afya cha Tinde. Ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ina mpango wa kuendelea kujenga yale majengo ambayo yanatakiwa pale kwa awamu ili kukamilisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kukamilisha majengo yale katika kituo cha afya cha Tinde, tutawa-consult wenzetu wa Wizara ya Afya ili waweze kukipandisha kwenda Hospitali hadhi ya Wilaya kulingana na uhitaji na vigezo ambavyo vitatimizwa katika kupewa kibali cha kupandisha kuwa Hospital ya Wilaya. (Makofi)
Name
Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Muleba kusini
Primary Question
MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Halmashauri ya Shinyanga?
Supplementary Question 5
MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru sana kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Wilaya ya Muleba ni kati ya Wilaya kongwe, na zenye watu wengi. Ninaishukuru Serikali kwa kutupatia ujenzi wa hospitali ya wilaya, lakini umekuwa ukidorora. Je, ni lini Serikali itamalizia na kutupatia pesa ya kutosha ili tukamilishe Hospitali ya Wilaya ya Muleba? (Makofi)
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu awali kwenye maswali madogo ya nyongeza, Serikali imefanya tathmini na tayari tumeshatenga bajeti kwa mwaka huu wa fedha 2026/2027 zaidi ya shilingi bilioni 56.25.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumetenga bilioni hizi ili kukamilisha ujenzi wa hospitali za wilaya 105. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, hiyo hospitali itakuwemo kwenye mpango huu na tutaweza kuikamilisha.
Name
Ester Amos Bulaya
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Halmashauri ya Shinyanga?
Supplementary Question 6
MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru. Nami niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa ninaishukuru TAMISEMI. Nilizungumza hapa kuwa kuna fedha zilirudi shilingi milioni 800, sasa mmezirudisha katika ujenzi wa hospitali yetu ya Halmashauri ya Mji wa Bunda, tunashukuru. Hata hivyo, hospitali bado haijakamilika, kuna majengo yanahitajika; kichomea taka, wodi ya watoto, bohari ya dawa na jengo la utawala. Vyote hivi vinagharimu takribani shilingi milioni 700.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini Serikali itatuletea fedha hiyo ili tukamilishe hospitali hiyo ya Halmashauri ya Mji, na wananchi waweze kupata huduma ya afya?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Mheshimiwa Mbunge anakiri kwamba Serikali ilipeleka fedha zile ambazo zilikuwa zimerudishwa ili kwenda kukamilisha baadhi ya miundombinu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tutaendelea kushirikiana kuhakikisha tunakamilisha na tunatenga bajeti kwa awamu kuendelea kukamilisha vichomea taka na yale majengo aliyoyataja ili kuweza kutoa huduma zinazotakiwa katika hospitali yetu hii.
Name
Amosy William Maganga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Sikonge
Primary Question
MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Halmashauri ya Shinyanga?
Supplementary Question 7
MHE. ENG. AMOSY W. MAGANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Tunaishukuru Serikali kwamba tunayo Hospitali ya Wilaya ya Sikonge, lakini haina uzio na kumekuwa na changamoto nyingi sana zinazosababishwa na kukosekana kwa uzio. Je, ni lini Serikali itatujengea uzio katika Hospitali yetu ya Wilaya ya Sikonge?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeendelea kusisitiza halmashauri, kwanza kufanya tathmini na kutenga fedha za kujenga uzio. Pia tutawasilisha maombi haya TAMISEMI, na kujiridhisha, kisha kuanza ujenzi wa uzio katika hospitali zote za halmashauri.
Name
Kija Limbu Ntemi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Katoro
Primary Question
MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Halmashauri ya Shinyanga?
Supplementary Question 8
MHE. KIJA L. NTEMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi na mimi niulize swali la nyongeza. Katika Hospitali ya Wilaya ya Katoro, tuna changamoto ya jenereta, limeharibika kwa muda mrefu, na huduma zimesimama. Lini sasa Serikali itapata jenereta ili kutimiza mahitaji ya wananchi katika Hospitali hiyo?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, hospitali hii ya wilaya inaendelea kutoa huduma kwa kutumia umeme wetu, lakini sasa huwa tuna yale majereta ya dharura ambapo sasa nimwelekeze Mkurugenzi afike eneo la tukio na aone kwanza namna gani ya kuweza kulirudisha jenereta lililokuwa linafanya kazi pale ili liendelee kuwa la dharura na kutoa huduma kwa wananchi wetu. (Makofi)