Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 9 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 88 | 2026-04-15 |
Name
Dr. Christina Christopher Mnzava
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: -
Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Halmashauri ya Shinyanga?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christina Christopher Mnzava, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Halmashauri ya Shinyanga ni miongoni mwa hospitali za awamu ya kwanza 68 zilizoanza kujengwa katika mwaka 2018/2019. Mpaka sasa jumla ya shilingi bilioni 3.49 zimeshatolewa kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Shinyanga ambapo jumla ya majengo 17 yamejengwa. Majengo mengine 10 yamekamilika na majengo saba yapo katika hatua ya ukamilishaji. Hospitali ya Halmashauri ya Shinyanga ilianza kutoa huduma Julai, 2020.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa miundombinu ya Hospitali umekuwa ukitekelezwa kwa awamu. Katika mwaka wa fedha 2026/2027 Hospitali ya Halmashauri ya Shinyanga imetengewa shilingi milioni 200 kwa ajili ya kukamilisha majengo saba yaliyosalia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa awamu kwa ajili ya kukamilisha miundombinu ya Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kama ilivyokusudiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved