Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO K.n.y. MHE ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- Je, ni miradi gani ya maji inatekelezwa Kyerwa, mkandarasi ni nani, inagharimu kiasi gani na lini itakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa kuwa miradi mingi ya maji kwenye Wilaya ya Kyerwa inachukua muda mrefu kukamilika kama ule Mradi wa Runyinya – Kimuli na wa vijiji 46; ni lini sasa Serikali itahakikisha kwamba inakamilisha miradi hii ili wananchi wa Kata ya Nyakantuntu na Kamuli waweze kunufaika? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Halmashauri ya Mji wa Tarime tunapata Mradi kutoka Ziwa Victoria, lakini tuliahidiwa kwamba tungeweza kupelekewa visima ambavyo vingeweza kusaidia kwenye maeneo kama ya Shule ya Sekondari Nyandoto, Nyakisese na Mkongole vilevile Vituo vya Afya vya Kibumayi na Magena; ni lini sasa Serikali itapeleka uchimbaji wa visima hivi wakati tukisubiria mradi mkubwa wa Ziwa Victoria? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI K.n.y. WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, lini tutakamilisha miradi hii ya vijiji 46 na huu mradi unaoenda kwenye hii Kata uliyoitaja Mheshimiwa Mbunge. Nikuhakikishie Serikali kadiri inapopata fedha tutahakikisha miradi hii inakamilika kwa sababu lengo la Serikali ni kuona wananchi wanapata maji safi na salama na kumpunguzia mwendo mwanamke ambaye anafuata maji umbali zaidi ya mita 400.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Tarime hivi visima navyo vipo katika mpango, Mheshimiwa Waziri naye anaendelea kuona namna ya njema ya kuhakikisha visima hivi tunakuja kuvichimba mapema sana na dhamira ya Mheshimiwa Rais ya kumtua mama ndoo kichwani inaweza kukamilika.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO K.n.y. MHE ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- Je, ni miradi gani ya maji inatekelezwa Kyerwa, mkandarasi ni nani, inagharimu kiasi gani na lini itakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Maji wa Kata ya Kikukuru mkandarasi ameondoka site zaidi ya miezi miwili kwa sababu ya madai; ni lini atalipwa ili arudi site kukamilisha mradi huu ambao ni muhimu kwa wananchi wa Kikukuru? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI K.n.y. WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza; lini mkandarasi atalipwa ili mradi ukamilike?

Mheshimiwa Spika, tayari Wizara imeanza malipo kwa wakandarasi wapo kwenye foleni wanapunguzwa taratibu na kadiri fedha inapopatikana tutahakikisha wakandarasi wote wanalipwa ili waweze kufanyakazi kadiri ya mikataba waliyosaini. (Makofi)

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO K.n.y. MHE ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- Je, ni miradi gani ya maji inatekelezwa Kyerwa, mkandarasi ni nani, inagharimu kiasi gani na lini itakamilika?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniona, mradi wa maji unaogusa Kata za Maji ya Chai – Kikatiti hadi Samaria Kata ya Maroroni inatekelezwa kwa kusuasua sana na katika ufuatiliaji wangu nimegundua kwamba mkandarasi pia mwenye matatizo kwa hiyo kuna haja ya kuchukua hatua stahiki mapema inavyowezekana.

Je, Waziri utakuwa tayari kuambatana na mimi twende jimboni tukafanye site meeting na stakeholders wote ikiwepo DC, Mkurugenzi na RUWASA? Nashukuru sana. (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI K.n.y. WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwanza mkandarasi yeyote ambaye hatekelezi majukumu yake anafahamu namna sheria ambavyo zinambana. Kwa hiyo, nikutoe hofu Mheshimiwa Mbunge naamini Wizara ya Maji wataenda kumshughulikia na kuona kwamba anafika site na kufanyakazi iliyotarajiwa.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kuambatana na yeye naomba nipokee na nitamfikishia Mheshimiwa Kundo naamini hatakuwa na kipingamizi katika hilo. (Makofi)