Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 26 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 334 | 2025-05-16 |
Name
Anatropia Lwehikila Theonest
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ESTHER N. MATIKO K.n.y. MHE ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:-
Je, ni miradi gani ya maji inatekelezwa Kyerwa, mkandarasi ni nani, inagharimu kiasi gani na lini itakamilika?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI K.n.y. WAZIRI WA MAJI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2024/2025, Serikali imekamilisha utekelezaji wa miradi miwili ya Nyamiaga-Nyakatera na Mabira kwa gharama ya shilingi 2,159,974,805.35 iliyopo Wilayani Kyerwa, Mkoa wa Kagera. Miradi hiyo imetekelezwa na wakandarasi wa ndani wa Kampuni za JAMTA Investment na AMRI AMIRI Co. Ltd. ambapo kwa sasa inanufaisha zaidi ya wakazi 26,123 waishio katika vijiji saba vya Masheshe, Nyamiaga, Kagu, Nyakatera, Mabira, Nyakatete na Omkagando.
Mheshimiwa Spika, vilevile Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi minne ya Runyinya - Chanya, Kaisho - Isingiro, Kimuli – Rwanyango - Chakalisa na Kikukuru - Rubirizi kupitia wakandarasi wa Makampuni ya JAMTA, SERENGETI na OTONDE kwa jumla ya gharama ya shilingi zaidi ya bilioni 13. Miradi hiyo ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji na inatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2025.
Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali imekamilisha uchimbaji wa visima vitano vya Jimbo la Kyerwa katika Vijiji vya Nyakatuntu, Nyakakoni, Songambele, Kamuli na Nyaruzumbura kupitia programu maalum ya uchimbaji wa visima 900. Kwa sasa kazi inayoendelea ni ufungaji wa pampu na ujenzi wa miundombinu rahisi ya kutolea huduma kwa wananchi inayotarajiwa kukamilika ndani ya mwezi Mei, 2025.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved