Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Condester Michael Sichalwe
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Momba
Primary Question
MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: - Je, lini Kituo cha Forodha katika Jimbo la Momba kitaanza kujengwa?
Supplementary Question 1
MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru, maboresho ya bandari zetu za Dar es Salaam pamoja na bandari nyingine ambazo shehena zake nyingi zinategemea kwenda nchi za SADC hususani kwa kupitia nchi ya Zambia ambapo ndiyo mlango mkubwa. Maboresho haya yameonekana kuwa na tija sana kiasi kwamba shehena kuongezeka na mpaka magari mengi kupungua kwa ajili ya kubeba mizigo, sidhani kama itakuwa ni sahihi tukiwa tunaendelea kuboresha tu bandari zetu na hatuboreshi mahali ambapo mzigo unakwenda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kutokana na maboresho ya bandari kumeleta tija, ni upi mkakati wa Serikali kuona kwamba kituo cha forodha peke yake cha Tunduma hakitoshei kusafirisha mizigo hiyo, hivyo kufanya mrundikano mkubwa sana wa magari pale Tunduma na upotevu mkubwa sana wa mapato?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, katika majibu yake ya msingi amesema ni lazima kuwe na mawasiliano na nchi ya pili, nilitaka kufahamu wameshaanza kuwashirikisha wenzetu wa Zambia kuona pale tulipoenda kumuonesha Waziri wa Fedha kipindi hicho ambaye ni Waziri Mkuu wa sasa. Je, wameshaparidhia kwamba panafaa kujenga kituo cha forodha katika Jimbo la Momba?
Name
Laurent Deogratius Luswetula
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kavuu
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. LAURENT D. LUSWETULA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mbunge wa Jimbo la Momba kwa kuendelea kuaminiwa na wananchi wake, unapokuwa unaaminiwa ni dhahiri ya kwamba unafanya ambayo ni matarajio ya wananchi, nikupongeze sana, lakini kwenye maswali ya nyongeza ninaomba nijibu kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nikutoe hofu kabisa Mheshimiwa Mbunge kwamba mazungumzo baina ya nchi hizi mbili yanaendelea vizuri na yana matumaini makubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye swali la pili la nyongeza, ni kweli kabisa Mamlaka ya Mapato Tanzania inaendelea na maboresho ya vituo vyetu vyote vya forodha kuhakikisha kwamba tunapokea mizigo mingi na kuipeleka sehemu ambayo inahitajika kwenye nchi jirani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo hivyo kwenye kituo chetu cha forodha cha Momba tumeendelea na kuboresha miundombinu kuhakikisha kwamba shehena nyingi na mizigo mingi inapita kuelekea kwenye hizo nchi jirani za SADC na kwa sababu hiyo nikuhakikishie kwamba sisi tumejipanga kuboresha miundombinu hiyo kuhakikisha meli zetu nyingi zinapita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo nimuagize Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwanza kuwarithisha tathmini hii ambayo ipo mwishoni kabisa na akishajiridhisha kwamba kuna ulazima wa haraka kabisa kuweza kujenga Kituo cha Forodha cha Kakozi basi nimwelekeze ujenzi huo uanze mara moja, ahsante sana. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved