Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 4 Finance Wizara ya Fedha 33 2026-04-08

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: -

Je, lini Kituo cha Forodha katika Jimbo la Momba kitaanza kujengwa?

Name

Laurent Deogratius Luswetula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. LAURENT D. LUSWETULA) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Fedha ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Condester Michael Sichwale, Mbunge wa Jimbo la Momba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa vituo vya forodha ikiwemo katika Jimbo la Momba hufanyika kwa kuzingatia vipaumbele vya Serikali, ukamilifu wa taratibu na kanuni za kiforodha, utayari wa nchi jirani tunazopakana nazo, masuala ya kiusalama, upatikanaji wa rasilimali fedha, pamoja na tathmini ya umuhimu wa eneo husika katika shughuli za biashara za mipakani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania inaendelea kufanya tathmini ya mahitaji ya ujenzi wa Kituo cha Forodha katika Jimbo la Momba ikiwemo upembuzi yakinifu, upatikanaji na utambuzi wa eneo, na gharama za mradi na utayari wa nchi jirani. Aidha, eneo hilo linaangaliwa kwa kuzingatia ongezeko la shughuli za biashara na umuhimu wake katika kuongeza ufanisi wa ukusanyaji wa mapato na udhibiti wa biashara mipakani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa kituo hicho utaanza mara baada ya kukamilika kwa maandalizi yote muhimu, ikiwa ni pamoja na kupatikana kwa fedha za utekelezaji wa mradi katika bajeti ya Serikali na kutangazwa kwenye Gazeti la Jumuiya ya Afrika Mashariki. Aidha, Mamlaka ya Mapato Tanzania inaendelea na maandalizi na itatoa taarifa rasmi pindi ratiba ya utekelezaji wa ujenzi itakapokamilika.