Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 4 | Finance | Wizara ya Fedha | 33 | 2026-04-08 |
Name
Condester Michael Sichalwe
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Momba
Primary Question
MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: -
Je, lini Kituo cha Forodha katika Jimbo la Momba kitaanza kujengwa?
Name
Laurent Deogratius Luswetula
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kavuu
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. LAURENT D. LUSWETULA) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Fedha ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Condester Michael Sichwale, Mbunge wa Jimbo la Momba kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa vituo vya forodha ikiwemo katika Jimbo la Momba hufanyika kwa kuzingatia vipaumbele vya Serikali, ukamilifu wa taratibu na kanuni za kiforodha, utayari wa nchi jirani tunazopakana nazo, masuala ya kiusalama, upatikanaji wa rasilimali fedha, pamoja na tathmini ya umuhimu wa eneo husika katika shughuli za biashara za mipakani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania inaendelea kufanya tathmini ya mahitaji ya ujenzi wa Kituo cha Forodha katika Jimbo la Momba ikiwemo upembuzi yakinifu, upatikanaji na utambuzi wa eneo, na gharama za mradi na utayari wa nchi jirani. Aidha, eneo hilo linaangaliwa kwa kuzingatia ongezeko la shughuli za biashara na umuhimu wake katika kuongeza ufanisi wa ukusanyaji wa mapato na udhibiti wa biashara mipakani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa kituo hicho utaanza mara baada ya kukamilika kwa maandalizi yote muhimu, ikiwa ni pamoja na kupatikana kwa fedha za utekelezaji wa mradi katika bajeti ya Serikali na kutangazwa kwenye Gazeti la Jumuiya ya Afrika Mashariki. Aidha, Mamlaka ya Mapato Tanzania inaendelea na maandalizi na itatoa taarifa rasmi pindi ratiba ya utekelezaji wa ujenzi itakapokamilika.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved