Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Suleiman Mohamed Rashid

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwera

Primary Question

MHE. SULEIMAN MOHAMED RASHID aliuliza:- Je, Serikali imejipangaje katika utekelezaji wa Sera ya Elimu ya Mwaka 2014 Toleo la 2023?

Supplementary Question 1

MHE. SULEIMAN MOHAMED RASHID: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na ninamshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini kipekee nimpongeze yeye pamoja na Mheshimiwa Waziri kwa namna ambavyo wanamsaidia Mheshimiwa Rais kwenye hili suala la elimu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni kwamba kutokana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia na mahitaji ya taaluma ya akili unde, Serikali imejipangaje ili taaluma hii kuweza kusomeshwa katika maskuli (shule)?

Name

Wanu Hafidh Ameir

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na kwa ruhusa yako ninaomba nimjibu Mheshimiwa Suleiman Mohamed Rashid, Mbunge wa Jimbo la Mwera, swali lake la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama vile ambavyo Serikali imejipanga katika utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014, ndivyo ambavyo Serikali imejipanga katika kuhakikisha kwamba kwa upande wa elimu ya akili unde, mikakati mbalimbali imeendelea kuchukuliwa. Kwa mfano, matumizi ya TEHAMA na teknolojia nyingine miongozo mbalimbali imetolewa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna miongozo imetolewa katika kutekeleza teknolojia za kidijitali katika elimu msingi, vyuo vikuu na vyuo vya ualimu. Pia kuna utekelezaji wa AI katika masomo, lakini pia Serikali imekuwa ikitoa ufadhili wa fursa za masomo ya nje ya nchi, lakini pia tumeendelea kuimarisha miundombinu ya elimu ya juu ili kuona kwamba mazingira ya watoto wetu ya kujifunzia yanaendana na mahitaji halisi ya teknolojia ikiwemo elimu ya akili unde. (Makofi)