Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 4 | Education, Science,Technology and Vocational Training, | Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia | 29 | 2026-04-08 |
Name
Suleiman Mohamed Rashid
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mwera
Primary Question
MHE. SULEIMAN MOHAMED RASHID aliuliza:-
Je, Serikali imejipangaje katika utekelezaji wa Sera ya Elimu ya Mwaka 2014 Toleo la 2023?
Name
Wanu Hafidh Ameir
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Suleiman Mohamed Rashid, Mbunge wa Mwera kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imejipanga kikamilifu katika utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014, Toleo la 2023 sambamba na mitaala iliyoboreshwa kwa kufanya yafuatayo:-
(i) Kuongeza miundombinu kwenye shule zilizopo;
(ii) Kuendelea na ujenzi wa shule mpya zikiwemo shule za mkondo wa Amali;
(iii) Kutoa mafunzo kazini kwa walimu ili kuendana na mahitaji ya mtaala mpya;
(iv) Kuimarisha uwiano wa kitabu kimoja kwa mwanafunzi katika ngazi ya elimu ya msingi na sekondari; na
(v) Kutoa ajira mpya za walimu ambapo katika mwaka 2024/2025 kibali cha ajira mpya 12,678 kilitolewa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, Serikali imezindua rasmi Mpango Mkakati wa Kisayansi wa Kujenga Umahiri wa Kusoma, Kuandika na Kuhesabu na Mpango wa Pamoja kati ya Waajiri, Vyuo vya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi na Vyuo Vikuu ili kuwawezesha wahitimu kuwa na ujuzi wa kujiajiri na kuajiriwa. Aidha, Serikali inafanya mapitio ya Sheria ya Elimu Sura 353 ili kuendana na mabadiliko ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 Toleo la 2023.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved