Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emanuel Qambaji Nuwas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. EMANUEL Q. NUWAS K.n.y. MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza: - Je, kwa nini Serikali isipitie upya Mkataba wa Shamba la Basotu la mwekezaji Ngano Limited lenye ukubwa wa ekari 43,000 ambalo limekuwa pori?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. EMANUEL Q. NUWAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa shamba hili ni shamba muhimu sana na limezungukwa na wananchi ambao wana uhitaji mkubwa, lakini pia wamekuwa wakipata changamoto, ninashukuru kupata majibu mazuri ya Serikali. Sasa wakati wa kampeni ya Mheshimiwa Rais aliahidi kwamba baada ya kampeni shamba hili litaweza kufanyiwa mapitio ili kuweza kufanyiwa uamuzi wa mwisho. Je, nini kauli ya Wizara?

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Waziri yuko tayari kufika katika Jimbo la Hanang ili kujionea mateso ambayo wanapata wananchi wanaozunguka shamba hili?

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, niaomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ambayo yameulizwa na Mbunge kutoka katika Mkoa wa Manyara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninachukua nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Asia Halamga kwa kazi kubwa anayoifanya. Mimi ni shahidi, amekuwa akiisumbua sana Serikali kuhusu haya mashamba mawili, shamba ambalo linamilikiwa na huyu mwekezaji Ngano Limited vilevile shamba ambalo kimsingi linasimamiwa na Serikali ya Halmashauri ya Hanang.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ninawahakikishia, watu wa Hanang hawakukosea kumchagua Mheshimiwa Asia Halamga na sisi kama Serikali tupo tayari kumpa ushirikiano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maelezo hayo, ninaomba kujibu maswali mawili kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, Rais alipoenda kufanya ziara pale Manyara alitoa commitment kwamba kwa kupitia taasisi yetu TISEZA kwamba tufanye tathmini ya kina tuone kama kuna haja ya kuendelea na yule mwekezaji au Serikali ichukue maamuzi mengine. Tayari sisi kama Serikali tulishanza kufanya tathmini na tunaendelea na hiyo tathmini.

Ninaomba nikuahidi, baada ya tathmini ile kukamilika tutatoa taarifa kwenye Kamati yetu ya Utawala, Katiba na Sheria, lakini Kamati yetu ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma ambako kimsingi TISEZA anaripoti ili vilevile muweze kupata taarifa na sisi kama Serikali tutachukua uamuzi wa haraka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, ninakubali kwamba baada ya Bunge hili tutafanya mkutano kule Manyara hususan katika Jimbo la Hanang pamoja na Mbunge ili tukasikilize kero za wananchi hususan wafugaji na wakulima katiKa Jimbo la Hanang, ninashukuru. (Makofi)