Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Saashisha Elinikyo Mafuwe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Hai
Primary Question
MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Afya Mnadani?
Supplementary Question 1
MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Mwenyekti, ahsante, kwanza ninaishukuru sana Serikali kwa majibu yake mazuri na ninapongeza watoa huduma kwa maana ya watumishi wa afya Wilaya ya Hai kwa kazi nzuri wanayoifanya wakiongozwa na Mkurugenzi wetu na DMO.
Swali la kwanza; Serikali ilituahidi kujenga Chuo cha Afya Narumu pamoja na kituo cha afya, tukahamasisha wananchi wakaanza ujenzi wa msingi na mimi kama Mbunge nikashiriki, je, ni lini sasa Serikali itatimiza ahadi yake hii?
Swali la pili, Wilaya ya Hai inavyo vituo, zahanati chakavu nne, zahanati chakavu kwa maana ya Uswaa, Mtakuja, Weruweru na Uroki. Serikali ina mpango gani mahsusi wa kukarabati zahanati hizi chakavu?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, Mbunge wa Jimbo la Hai.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninampongeza sana Mbunge kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuwapambania wananchi wa Jimbo la Hai na hakika ziara ya Waziri Mkuu tuliifuatilia wote na Waziri Mkuu alisema kweli Hai imepata Mbunge wa uhakika, smart boy.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba kwanza tunawashukuru wananchi wa Jimbo la Hai kwa nguvu zao ambazo walitumia kupata eneo hilo na kuanza ujenzi, pia ninampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kutenga Mfuko wa Jimbo kuona tunasukuma mbele gurudumu la maendeleo ya afya katika Jimbo la Hai. Ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusu zahanati, nikuhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali tumekwishatenga bajeti ya kuanza kuboresha zahanati zile chakavu hasa zile za zamani. Kwa hiyo, katika Jimbo la Hai na lenyewe tutalipa kipaumbele kutenga bajeti hizi za kuboresha miundombinu ya zahanati zile za zamani. Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wa Jimbo la Hai, tunawahakikishia kwamba Serikali itaendelea kupeleka fedha kadri tunavyozipata.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha. (Makofi)
Name
Sikudhani Yasini Chikambo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Afya Mnadani?
Supplementary Question 2
MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, awali ya yote kwanza ninapenda kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyenijaalia afya njema na kuwa sehemu ya Wabunge katika Bunge lako hili, haikuwa rahisi lakini kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu hakuna kinachoshindikana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, miongoni mwa kata zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ni pamoja na Kata ya Kidodoma. Kata ile ina vijiji vitano lakini mpaka hivi tunavyozungumza ile kata haina kituo cha afya na mpango wa Serikali ni kuhakikisha tunakuwa na vituo vya afya katika kila kata.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninatamani kujua, ni nini mkakati wa Serikali katika kuhakikisha tunapata kituo cha afya katika Kata ile ya Kidodoma? Ahsante.
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sikudhani kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa Serikali ni kuhakikisha tunajenga vituo vya afya kila kata. Bunge lako Tukufu liliridhia kuanza na vituo vya afya vya kimkakati, ambapo tayari tumekwishajenga vituo vya afya 120 na tayari tumekwishaomba fedha kwa ajili ya kujenga vituo vingine vya afya vya kimkakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamhakikishia Mbunge kwamba katika eneo hili la kituo cha afya, kwanza wanazo zahanati ambazo zinaendelea kutoa huduma, lakini na wenyewe tutaweka katika kipaumbele ili tuweze kuwajengea kituo cha afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha. (Makofi)
Name
Husna Juma Sekiboko
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Afya Mnadani?
Supplementary Question 3
MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru, Kituo cha Afya Kwekanga ni kituo cha kimkakati lakini ujenzi wake umechukua muda mrefu sana. Tunaomba majibu ya Serikali, ni lini Serikali itapeleka fedha kwenye Kituo cha Afya Kwekanga katika Wilaya ya Lushoto kwa ajili ya ukamilishaji wa majengo katika kituo hicho?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sekiboko, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vituo vya afya ambavyo tayari vilishatengewa fedha na vikapelekewa zile shilingi milioni 250, Serikali inatambua siyo kwamba zile shilingi milioni 250 tayari zinatosheleza, tumekwishawaelekeza Wakurugenzi, hasa kwenye zile halmashauri zenye mapato makubwa ili waweze kuendelea kuboresha miundombinu ambayo itaendelea kutoa huduma kwa watu wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali tunaendelea kulichukua jukumu hili ili kuona vituo vyote ambavyo tumevianzisha vinakamilika na vinatoa huduma kwa wananchi wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha. (Makofi)
Name
Kunti Yusuph Majala
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Afya Mnadani?
Supplementary Question 4
MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kuniona na mimi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kata ya Mpendo, Jimbo la Chemba ni kata iliyoko pembezoni lakini kata hii ina zahanati moja tu ambayo inatoa huduma kwa vijiji vinne. Nini mkakati wa Serikali wa kuwajengea kituo cha afya wananchi wa Kata ya Mpendo?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Mheshimiwa Kunti kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mkakati wa Serikali ni kuhakikisha tunajenga vituo hivi vya afya na katika jimbo hili tutawapa kipaumbele ili kuona namna gani tunaanza ujenzi wa kituo hiki katika kipindi hiki cha fedha. Katika miaka hii kuanzia Bunge hili la mwaka 2026 mpaka mwaka 2027 tutaona namna ya kuboresha na kujenga kituo hicho cha afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha. (Makofi)
Name
Juma Ramadhani Mustafa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Igalula
Primary Question
MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Afya Mnadani?
Supplementary Question 5
MHE. JUMA R. MUSTAFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza kwenye Wizara ya TAMISEMI. Kwanza kabisa ninapenda kuipongeza Serikali kwa kazi nzuri ambazo inaendelea kufanya.
Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya umaliziaji wa maboma ya vituo vya afya vilivyomo ndani ya Jimbo la Igalula? Vituo hivyo vilivyopo ndani ya Jimbo la Igalula ni Kata ya Tura, Goweko, Kizengi, Lutende na Loya, kwani ndani ya Jimbo la Igalula hatuna hata kituo kimoja cha afya kilichokamilika majengo. Tunaiomba Serikali itusaidie kutupelekea fedha.
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kawamba, Mheshimiwa Mbunge wa Igalula na ninampongeza sana ndugu yangu kwa kufuatilia hali na mahitaji ya wananchi wa Jimbo la Igalula.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie na hata Bunge lililopita nilimhakikishia kwamba tutakwenda kuhakikisha tunaboresha maeneo haya ya vituo vya afya, tunamalizia maboma ambayo bado yameonekana ni changamoto ili kuweza kutoa huduma katika Jimbo la Igalula na Wana-Igalula waweze kupata tabasamu la Mheshimiwa Dkt. Samia Samia Suluhu Hassan. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha.
Name
Yohana Stephen Msita
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Itigi
Primary Question
MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Afya Mnadani?
Supplementary Question 6
MHE. YOHANA S. MSITA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, nami kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Itigi ninapenda kumuuliza Mheshimiwa Waziri.
Kwa kuwa Jimbo la Itigi lina kata 13 na tunavyo vituo vinne tu vya afya na hili jimbo lipo scattered sana. Je, nini mpango wa Serikali kujenga vituo vya afya angalau kwenye kata tatu za Ipande, Mgandu pamoja na Mwamagembe ili kupunguza adha ya wananchi wangu? (Makofi)
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Yohana, Mbunge wa Jimbo la Itigi kama ambavyo ameliuliza. Jimbo la Itigi ni miongoni mwa majimbo ambayo tumekwishayaombea fedha Hazina ili tuweze kujenga vile vituo vya afya vya kimkakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge nitampa ushirikiano wa dhati ili kuweza kuhakikisha angalu kwenye kata hizi tatu alizoziainisha ziweze kupata kituo cha afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha. (Makofi)