Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fadhili Sandali Chilombe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. ENG. FADHILI S. CHILOMBE aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara za kuunganisha vijiji vilivyoanzishwa toka mwaka 1974 katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. FADHILI S. CHILOMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini naomba kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Tunduru, hususan Jimbo la Tunduru Kusini ina vijiji vingi ambavyo bado pamoja na jitihada za Serikali za kufungua, lakini hivyo vijiji havijawahi kupata hizo barabara. Mimi nafananisha barabara kama uwepo wa mishipa ya damu kwenye mwili wa binadamu kwamba ili tu-speed up maendeleo tunatakiwa pale sehemu ambapo tunaweza tukatengeneza ukaribu wa vijiji kuwasiliana ikafanywa hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninatoa mfano, kipo Kijiji cha Semen na Kijiji cha Chiwana au kuna Kijiji kinaitwa Nalasi na Kijiji cha Mnemasi. Ukitoka Semen kwenda Chiwana ipo shortcut ya kilometa tano tu, lakini hivi tunavyoongea leo, ili kukifikia kijiji hicho unahitaji kutembea kilometa 17. Sasa swali je, Serikali haioni umuhimu wa kuhakikisha kwamba vile vijiji ambavyo vinakaribiana kwa mtindo huo vinafanyiwa sasa? Hilo swali langu la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, ipo barabara inatokea Chiungo inapita Mkambara inaenda mpaka Mkasale. Barabara hii ilifunguliwa zaidi ya miaka 10 iliyopita, kinachoombwa sasa ni ile barabara kusajiliwa ili iweze kupata huduma ya TARURA na ukitoka hapa Mkambara kwenda Mkasale ni kilometa zisizozidi nne katikati pale pana mto ambao huwa unajaa, sasa wananchi wa Mkambara wanategemea Hospitali ya Mkasale.

Je, Serikali itakamilisha lini jambo la kuisajili ile barabara kwa sasa? (Makofi)

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naanza kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Fadhili, engineer huyu. Kwa bahati nzuri nilifika katika Jimbo lake na tulifanya mkutano mkubwa sana pale jimboni na wananchi wa Jimbo la Tunduru Kusini pamoja na Tunduru Kaskazini ni waungwana sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge, maswali yake mawili ya nyongeza. Hili la kilometa tano nawaelekeza TARURA kuanzia sasa wafike eneo hili kufanya tathmini katika shortcut hii na kuweza kuitengea bajeti ya kuanza utekelezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kusajiliwa; tuna utaratibu wa kusajili barabara hizi katika Wakala wetu wa TARURA na pia nawaelekeza Meneja wa TARURA wa Mkoa pamoja na yule wa Wilaya waweze kuisajili barabara hii iweze kutoa huduma kwa watu katika Jimbo la Tunduru Kusini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha. (Makofi)

Name

Agnesta Lambert Kaiza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. FADHILI S. CHILOMBE aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara za kuunganisha vijiji vilivyoanzishwa toka mwaka 1974 katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Supplementary Question 2

MHE. AGNESTA L. KAIZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya kutoka Baracuda kupitia Chang’ombe kupitia Majichumvi kwenda kule Majumba Sita ni zaidi ya mwaka sasa imepata mkandarasi. Huyo mkandarasi alichofanya ni kwenda kuweka bango lake la ukandarasi pale, mpaka hivi sasa ninavyoongea hakuna chochote kinachoendelea kwenye hiyo barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kufahamu siku ya leo, ni lini ujenzi wa hiyo barabara utaanza? Zingatia ni lini ujenzi huo utaanza? Ahsante sana.

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Agnesta Kaiza, kama alivyoliuliza.

Kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Agnesta Kaiza kwa kuwapambania wanajimbo la Segerea na amezitaja barabara kama alivyoziainisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii tayari inaye mkandarasi, anachosubiri ni advance payment ili aweze kuanza kufanyakazi. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge, barabara hii itaweza kuanza kujengwa katika bajeti hii kadri tunavyoendelea kupata fedha na kumlipa mkandarasi aweze kuanza kufanya utekelezaji huo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha. (Makofi)

Name

Haran Nyakisa Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. ENG. FADHILI S. CHILOMBE aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara za kuunganisha vijiji vilivyoanzishwa toka mwaka 1974 katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Supplementary Question 3

MHE. HARAN N. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza napenda kuipongeza Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutupa mtandao wa barabara kilometa kama 45, lakini naomba niulize swali tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepata wakandarasi sita ambao wanatekeleza utengenezaji wa zile barabara za DMDP, lakini toka nimefanya ziara ni miezi minne sasa hivi wameingia site, wengine wameweka vifaa, lakini hawapo site hadi sasa hivi tunavyoongea hapa na kila ukiwauliza wanazungumza wanasema labda fedha hazijatoka.

Sasa tunaomba kauli ya Serikali, ili wananchi wale waweze kupunguziwa adha ya zile barabara walizokuwa wamezitindua maana zinakwamisha upitaji. (Makofi)

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Sanga, Mbunge wa Kigamboni na bahati nzuri alipata ziara ya Waziri wetu, alifika kule na akajionea barabara hizi. Pia namhakikishia Mheshimiwa Sanga, mimi na yeye baada ya hapa tuwasiliane ili tuone fedha hizi ambazo Serikali imeshazielekeza kwa ajili ya ujenzi wa barabara hizi kilometa 45. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha. (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. FADHILI S. CHILOMBE aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara za kuunganisha vijiji vilivyoanzishwa toka mwaka 1974 katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Supplementary Question 4

MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa mvua inayoendelea ina mchango mkubwa katika uharibifu wa miundombinu ya barabara Kata ya Mapinga, Nianjema na Kisutu, Jimbo la Bagamoyo. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri upo tayari ukipata fursa ya kutembelea maeneo hayo ili kuona zile fedha za TARURA na kuelekeza maeneo korofi ikiwemo mifereji ili maji yaweze kwenda baharini na kuwaacha wananchi katika maeneo ya nchi kavu? (Makofi)

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza kwa ujumla, ni kwamba tumepata changamoto ya mvua hizi katika maeneo mengi nchini likiwemo Jimbo langu mwenyewe la Busanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepata changamoto ya mvua katika maeneo yote na yale ambayo Mheshimiwa Mbunge ameainisha. Mimi niko tayari kuongozana na Mheshimiwa Mbunge katika maeneo haya kwenda kufanya tathmini, lakini pia kuwaelekeza TARURA kujenga miundombinu ambayo itakua ni himilivu katika kipindi hiki kwa kadri tunavyopata vipindi vya mvua ili miundombinu iweze kuwa himilivu.