Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 4 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 22 | 2026-04-08 |
Name
Fadhili Sandali Chilombe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduru Kusini
Primary Question
MHE. ENG. FADHILI S. CHILOMBE aliuliza:-
Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara za kuunganisha vijiji vilivyoanzishwa toka mwaka 1974 katika Jimbo la Tunduru Kusini?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Fadhili Sandali Chilombe, Mbunge wa Tunduru Kusini, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa kuunganisha vijiji vyote 65 vilivyopo katika Wilaya ya Tunduru ili kuchochea ukuaji wa shughuli za kiuchumi na kufikisha huduma za kijamii. Katika kutekeleza azma hiyo, Serikali imeendelea kuhudumia mtandao wa barabara wenye jumla ya kilometa 1,203.61 katika Wilaya ya Tunduru ambapo maeneo ya Jimbo la Tunduru Kusini pia yamepewa kipaumbele.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuunganisha vijiji ambavyo havijafikiwa tangu mwaka 1974, Serikali kwa kutumia fedha za maendeleo ya jimbo na nyongeza ya tozo ya mafuta imeendelea kufungua barabara za kuunganisha vijiji. Mpaka sasa imeshafungua barabara mpya zenye urefu wa kilometa 117.7 ambapo shilingi bilioni 1.25 zimetumika kufungua Barabara za Semen – Tupendane – Mchesi, Nalasi – Nasomba – Lukala, pia Barabara ya Chikomo – Mkandu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mtandao wa barabara wa TARURA ni kilometa 144,149.18 ambapo Serikali inaendelea kupanua mtandao huu, ili kuwezesha kufikia maeneo mbalimbali, ikiwemo ya vijijini. Kadri Serikali inavyojenga uwezo wa kibajeti wa wakala itawezesha maeneo mengi nchini kufikiwa, vikiwepo vijiji vilivyoanzishwa toka mwaka 1974 katika Jimbo la Tunduru Kusini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved