Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bakari Bakari Shingo

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. BAKARI B. SHINGO aliuliza: - Je, Serikali haioni haja kukemea vitendo vya kutoza gharama za matibabu kwa wajawazito na watoto chini ya miaka mitano?

Supplementary Question 1

MHE. BAKARI B. SHINGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Serikali inaandaa mpango kwa ajili ya bima za afya. Swali langu lilikuwa linazungumzia kipindi hiki ambacho bima hiyo ya afya kwa wote haijaanza kukamilika, na huku tukijua kwamba nyuma kuna sera ya wazee kuhudumiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jimbo langu, kuna wazee kadhaa wameshindwa kupata hiyo huduma. Swali langu linasimama kwamba, hawana sifa ya kupata huduma hiyo wakati tukisubiri mpango huo wa Bima ya Afya kwa Wote?

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge wa Ukonga Mheshimiwa Bakari Bakari kwa kuwa kinara wa kutetea afya za akina mama wa Tanzania ili waweze kujifungua na kuwa salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya Bima ya Afya kuanza, Serikali ilikuwa na utaratibu maalum ambao wagonjwa hawa wa makundi maalum wakiwemo wajawazito, akina mama, watoto, na wazee walikuwa wanagharamiwa matibabu na Serikali bure kwa kupelekewa vifaa na kwa kupewa msamaha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikitumia zaidi ya shilingi bilioni 40 kwa mwaka kuwahudumia wagonjwa hawa kwa kutoa msamaha katika hospitali zetu. Wanapewa vipimo, wanapewa matibabu, wanajifungua kwa gharama za hospitali. Hii ndiyo imepelekea vifo vya mama na mtoto kupungua katika nchi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa namna ya pekee kabisa, nimpongeze Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan Suluhu Hassan ambaye aliamua kuwekeza kwenye idara hii ya mama na mtoto. Tumeona vifo vikipungua kwa zaidi ya 80%. Vifo vimetoka 556 kwa vizazi hai 100,000 mpaka vifo 104 kwa vizazi hai 100,000, hali iliyopelekea mpaka Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan Suluhu Hassan kutunukiwa tuzo ya Goal Keeper Award na Gates Foundation ambayo haijawahi kutokea kwa Rais yeyote mwananamke duniani kupewa tuzo hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haijawahi kutokea Rais yeyote Afrika kupewa tuzo hii. Yeye akiwa ni Rais wa kwanza Tanzania kupewa tuzo hii kwa sababu kwa moyo wa dhati kabisa amewekeza katika kumhudumia mama na mtoto ili kupunguza vifo hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayo malengo mkakati, ifikapo mwaka 2030 tunataka kupunguza vifo vya mama na mtoto mpaka kufikia vifo 70 kwa kila vizazi hai 100,000. Ndiyo maana tumekwenda kwa Bima ya Afya kwa Wote ili sasa kuwa na huduma bora zaidi kwa ajili ya akina mama waweze kujifungua salama na watoto wao waendelee kuwa salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.