Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 6 | Health and Social Welfare | Wizara ya Afya | 106 | 2026-02-03 |
Name
Bakari Bakari Shingo
Sex
Male
Party
ACT
Constituent
Ukonga
Primary Question
MHE. BAKARI B. SHINGO aliuliza: -
Je, Serikali haioni haja kukemea vitendo vya kutoza gharama za matibabu kwa wajawazito na watoto chini ya miaka mitano?
Name
Dr. Florence George Samizi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Muhambwe
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bakari Bakari Shingo, Mbunge wa Ukonga kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatekeleza Sera ya Afya ya Mwaka 2007 inayoelekeza kutoa huduma za matibabu bure kwa makundi maalum ikiwemo akina mama wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka mitano pamoja na wazee wenye umri zaidi ya miaka 60 wasio na uwezo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeshatangaza rasmi kuanza utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa wote awamu ya kwanza itakayohusisha makundi ya wananchi ikiwa ni pamoja na watoto, wajawazito, walemavu na wazee wasio na uwezo, ambapo kundi hili litagharamiwa na Serikali. Kukamilika kwa hatua hii kutawezesha wajawazito na watoto chini ya miaka mitano kupata huduma za afya kwa kugharamiwa na Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, natoa rai kwa waganga wakuu wa mikoa na wilaya pamoja na waganga wafawidhi wa vituo vya kutolea huduma za afya kuhakikisha kuwa wanatekeleza maelekezo ya Serikali katika kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma za afya kikamilifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved