Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Japhael Masanja Lufungija
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ulyankulu
Primary Question
MHE. JAPHAEL M. LUFUNGIJA K.n.y. MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: - Je, kwa nini Mkulima analazimika kununua mbegu za mahindi kila mwaka badala ya kutumia zile ambazo amevuna?
Supplementary Question 1
MHE. JAPHAEL M. LUFUNGIJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Serikali, ninayo maswali mawili ya nyongeza kwa niaba ya Mheshimiwa Margaret Sitta.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kilimo cha mahindi ni zao la mkakati katika nchi yetu, na ni zao linalolimwa na wananchi wengi, wakiwepo wananchi maskini na hasa wale ambao wanahudumiwa na Serikali, kwa maana ya TASAF, ukilinganisha gharama ya mbegu kwa wastani kilo mbili za mbegu zinanunuliwa kwa shilingi 15,000 kwa maana ya ekari moja inatumia mifuko minne kwa thamani ya shilingi 60,000, ukijumlisha pamoja na mbolea na gharama za kilimo inapelekea wastani wa heka moja cost yake kama 350,000, je, Wizara ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba gharama ya mbegu inashuka ili kuweza kuzibeba na familia maskini ziweze kulima vizuri zao la mahindi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Katika Mkoa wa Tabora, na hasa kwenye Jimbo la Urambo, Ulyankulu, Kaliua na majimbo mengine, lipo tatizo la wadudu waharibifu wa mahindi hasa yakiwa na kina kuanzia futi moja mpaka futi tano. Wadudu wanaitwa al-maarufu rusomi, wanashambulia sana mahindi na kuyaharibu. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba dawa za kuwatibu wadudu wale zinaingia kwenye ruzuku?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, ameuliza maswali ya msingi kwa niaba ya Mheshimiwa Mama Sitta. Nimwambie tu kwamba moja ya mpango wa Serikali katika kupunguza gharama kwa mkulima ni pamoja na kuweka ruzuku. Miongoni mwa ruzuku tulizoweka, tumeweka ruzuku katika mbegu, lakini vilevile tumeweka ruzuku katika mbolea na viuatilifu, lengo tu ni kupunguza gharama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, bado Serikali tumeendelea na mikakati ya kuhakikisha kwamba uzalishaji wa mbegu unaongezeka. Ndiyo maana sasa hivi kwa wakulima ambao wanataka kuingia katika kile kilimo cha kimkataba katika mashamba ambayo yanamilikiwa na Wakala wetu wa Uzalishaji wa Mbegu (ASA), tumekuwa tukiruhusu watu kuingia katika kilimo cha kimkataba ili tuongeze uzalishaji wa mbegu hapa nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba bado tunaendelea na michakato ya kuhakikisha kuwa tunaongeza uzalishaji ili tuhakikishe kuwa bei inashuka pamoja na kwamba tumeweka ruzuku ndani yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hawa wadudu waharibifu ambao ameainisha, watu wetu wa TPHPA wanaendelea na hiyo kufanya tathmini kwa sababu uwekaji wa ruzuku katika viuatilifu ni hatua kwa hatua. Kwa hiyo, tumeweka sehemu katika mazao kama ya parachichi, tumeweka sehemu katika mazao ya korosho na vilevile tutaangalia katika wadudu waharibifu wa mahindi. Kwa hiyo, na lenyewe lipo katika mchakato na tukishalikamilisha tutatolea taarifa hapa. Ahsante sana.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved