Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 6 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 105 | 2026-02-03 |
Name
Margaret Simwanza Sitta
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Urambo
Primary Question
MHE. JAPHAEL M. LUFUNGIJA K.n.y. MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: -
Je, kwa nini Mkulima analazimika kununua mbegu za mahindi kila mwaka badala ya kutumia zile ambazo amevuna?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkulima hulazimika kununua mbegu kila msimu ili aweze kupata tija iliyodhamiriwa kwa sababu mbegu anazonunua katika maduka ya pembejeo huwa zimepitia majaribio ya kisayansi katika maabara ili kuthibitisha ubora wa sifa mbalimbali, ikiwemo kiwango cha uzalishaji, uhimilivu wa magonjwa na ukame. Mkulima anapovuna mazao na kutumia kama mbegu kwa mara ya pili au zaidi husababisha sifa za mwanzo za mbegu husika kupungua ama kupotea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, asilimia kubwa ya mbegu zinazotumiwa na wakulima nchini, ni mbegu aina ya chotara ambazo utengenezaji ama uzalishaji wake hutumia aina mbili au zaidi tofauti za mbegu wazazi kutoka jamii moja. Kutokana na sababu hiyo, iwapo mbegu hizo zitatumika kama mbegu kwa mara ya pili au zaidi husababisha kupotea au kupungua kwa sifa bora za mbegu hivyo kuchangia kushuka kwa tija na uzalishaji wa mazao ya mkulima.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved