Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emanuel Qambaji Nuwas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. EMANUEL Q. NUWAS K.n.y. MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga barabara ya Karatu – Mbulu – Haydom – Lalago kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. EMANUEL Q. NUWAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Ninashukuru sana kwa kazi nzuri ambayo inafanywa na Serikali na kazi inaendelea, lakini bado speed siyo kubwa. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza. Tuna wananchi ambao barabara imewafuata kwa upande wa Mbulu – Garbabi na Labay – Haydom. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kuwalipa fidia wananchi hawa na kumwezesha mkandarasi kuikimbiza hii kazi kwa wakati? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Tuna kipande cha Garbabi – Dongobesh – Labay, kilometa 35, ambayo bado mchakato wake haujaanza, na Barabara hii inategemewa sana na wakulima wa kilimo cha umwagiliaji. Je, ni lini Serikali itaanza mchakato wa ujenzi wa kipande hiki cha katikati? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hawa wananchi ambao barabara imewafuata, ninaomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutahakikisha wanalipwa kabla hawajaondolewa kwenye maeneo yao ambayo barabara imewafuata. Kwa hiyo, tutahakikisha, kwa sababu barabara tumeshaanza kuijenga, na ili tujenge, ni lazima tuwalipe. Kwa hiyo, niwahakikishie tutawalipa hiyo fidia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu eneo la Garbabi – Dongobesh, ninadhani ndiyo barabara ambayo inaenda Dareda. Tumeshaanza upande wa Dareda Mission, tunajenga, na tutahakikisha tunaikamilisha hiyo barabara kwa kiwango cha lami, kadri fedha itakavyokuwa inapatikana. (Makofi)