Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 6 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 101 2026-02-03

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. DKT. EMANUEL Q. NUWAS K.n.y. MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga barabara ya Karatu – Mbulu – Haydom – Lalago kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itajenga barabara ya Karatu – Mbulu – Haydom – Lalago kwa kiwango cha lami kwa awamu. Hadi sasa, taratibu za manunuzi ya mkandarasi wa ujenzi wa sehemu ya Nkoma – Lalago, kilometa 65 zimekamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, kwa sehemu ya Mbulu – Garbabi, kilometa 25, kazi za ujenzi zinaendelea na zimefikia 41% na kwa sehemu ya Labay – Haydom, kilometa 25 kazi za ujenzi zimefikia 11%. (Makofi)