Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kellen Rose Rwakatare

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. KELLEN R. RWAKATARE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kutoka Daraja la Lumemo - Mbingu – Chita?

Supplementary Question 1

MHE. KELLEN R. RWAKATARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza. Je, ni lini Serikali imejipanga kukamilisha hayo malipo ya awali (advance payment) ili ujenzi uanze kufanyika kwa speed, kwa sababu wananchi wa Mlimba wamesubiri sana kwa muda mrefu?

Je, ni lini Mheshimiwa Naibu Waziri atapanga muda ili tuambatane kwa pamoja ili kujionea mwenyewe mazingira na hali halisi ilivyo ya barabara za Jimbo la Mlimba zilivyo? Mvua zinanyesha kwa wingi, barabara zina makorongo, hazipitiki na wananchi wanapata taabu sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninataka kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tumeshapata mkandarasi, tunajua athari ya kutokumlipa malipo ya awali. Malipo ya awali yanaandaliwa ili aweze kuanza kazi ya ujenzi kwa kipande hicho cha kilometa 37.5. Kwa hiyo, ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba mkandarasi ameshapatikana na atalipwa malipo ya awali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kutembelea hiyo barabara, ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge, niko tayari. Ninakuhakikishia nimeshaitembea hiyo barabara mara mbili, kuanzia Ifakara – Mbingu – Mlimba – Kibena Junction. Kwa hiyo, ninaifahamu, ni barabara muhimu ambayo inaunganisha Njombe na Morogoro. Kwa hiyo, niko tayari, ahsante. (Makofi)

Name

Zacharia Paulo Issaay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. KELLEN R. RWAKATARE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kutoka Daraja la Lumemo - Mbingu – Chita?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Je, ni lini Serikali itatekeleza ujenzi wa barabara ya Magara – Mbuyuni – Mbulu kwa kiwango cha lami ambapo ni ahadi ya Makamu wa Rais kwa miaka mitano sasa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, hii barabara ni kweli inapita kwenye escapement ambapo tunachokifanya sasa hivi ni kujenga kiwango cha zege kwenye ile miinuko mikali ili magari yaweze kupita wakati tunatafuta fedha, lakini kikubwa atakubaliana na mimi kwamba lile Daraja la Magara tulishalikamilisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali tunaendelea kutafuta fedha kuijenga barabara yote kwa kiwango cha lami, lakini kikubwa sasa ni kujenga kwa kiwango cha zege kwenye ile miinuko mikali. (Makofi)