Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 6 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 100 2026-02-03

Name

Kellen Rose Rwakatare

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. KELLEN R. RWAKATARE aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kutoka Daraja la Lumemo - Mbingu – Chita?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya kuanzia Daraja la Lumemo – Mbingu – Chita ni sehemu ya barabara ya Ifakara – Njombe Border yenye urefu wa kilometa 220. Ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa, ujenzi umeanza sehemu ya Ifakara – Mbingu, kilometa 62.5. Aidha, kwa sehemu ya Mbingu – Chita, urefu wa kilometa 37.5, mkandarasi amepatikana na taratibu za malipo ya awali advance payment zinaendelea ili aweze kuanza kazi, ahsante.