Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 6 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 100 | 2026-02-03 |
Name
Kellen Rose Rwakatare
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Mlimba
Primary Question
MHE. KELLEN R. RWAKATARE aliuliza: -
Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kutoka Daraja la Lumemo - Mbingu – Chita?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya kuanzia Daraja la Lumemo – Mbingu – Chita ni sehemu ya barabara ya Ifakara – Njombe Border yenye urefu wa kilometa 220. Ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa, ujenzi umeanza sehemu ya Ifakara – Mbingu, kilometa 62.5. Aidha, kwa sehemu ya Mbingu – Chita, urefu wa kilometa 37.5, mkandarasi amepatikana na taratibu za malipo ya awali advance payment zinaendelea ili aweze kuanza kazi, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved