Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Silvery Luboja Salvatory
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Misungwi
Primary Question
MHE. SILVERY L. SALVATORY aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza Mradi wa Maji Bonde la Lujamate –Buhingo ambao umesimama kwa muda mrefu?
Supplementary Question 1
MHE. SILVERY L. SALVATORY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa wananchi wa vijiji 16 vya Gukwa Buhunda, Mwagimagi, Kifune, Busongo, Nyambiti, Kabale, Buhingo, Seke, Songiwe, Mwasagela, Mbalama, Nyamayinza, Gulumungu, Ng’hamve pamoja na Itogwang’holo viko kwenye Mradi wa Maji wa Ihelele unaopeleka maji Mikoa ya Shinyanga na Tabora, na unaanzia kilometa zero kutoka kwenye chanzo cha maji; Tangu uzinduliwe mwezi Juni, 2009 wananchi hawa hawajawahi kupata maji ilhali maji yananyewa Sikonge. Je, sasa Serikali haioni ni wakati umefika wananchi hawa na wao waweze kupewa maji kwa haraka?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Kwa kuwa maji ni uhai, je, Serikali ina mkakati gani wa dharura wa kuwapatia wananchi hawa maji kwa haraka ili kuokoa afya zao? Ninakushukuru.
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Salvatory, Mbunge wa Misungwi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa kwenye upande wa Misungwi Serikali imefanya kazi kubwa sana. Upatikanaji wa maji wa sasa wa Misungwi ni 68%, lakini Serikali imetekeleza zaidi ya miradi 15 na yenye gharama ya shilingi bilioni 15.6, lakini miradi inayoendelea kwa sasa ni nane yenye gharama ya shilingi bilioni 69. Hii ni kazi kubwa inayofanywa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Jimbo la Misungwi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua kwamba kazi ya Serikali ni kuhakikisha kwamba vijiji vyote vinapata huduma ya majisafi na salama, lakini kati vijiji 94 vyote tayari vina maji na vijiji vinane ndivyo ambavyo bado tunahakikisha kwamba mradi huu unaoendelea utakapokamilika pamoja na vile vijiji 16 vyote vitapata huduma ya majisafi na salama. Tunafahamu kwamba maji ni uhai, lakini maji ni uchumi. Tunafahamu kwa kuwawezesha wananchi wa Misungwi wataweza kufanya shughuli zao za kiuchumi, lakini pia wataweza kutumia majisafi na salama kwa ajili ya kunywa, ahsante sana.
Name
Edward Olelekaita Kisau
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kiteto
Primary Question
MHE. SILVERY L. SALVATORY aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza Mradi wa Maji Bonde la Lujamate –Buhingo ambao umesimama kwa muda mrefu?
Supplementary Question 2
MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa nafasi. Mheshimiwa Naibu Waziri Mradi wa Nchinilai – Engusero umechukua muda mrefu sana na unasuasua sana. Ni lini Naibu Waziri yuko tayari, kwa siku ambazo siyo nyingi sana tutembelee mradi huu ili tupate majibu ya uhakika?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Olelekaita, na hakika tunapokuwa katika ziara jimboni kwake anatupatia ushirikiano mzuri sana, na pia tunapohitaji taarifa za maendeleo ya miradi yetu ndani ya jimbo lake anatupatia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hivyo, nipo tayari kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji kwenda kutembelea mradi huu na kuupa push ili uweze kukamilika na wananchi wake wa Kiteto wapate huduma ya majisafi na salama, ahsante sana.
Name
Bakari Bakari Shingo
Sex
Male
Party
ACT
Constituent
Ukonga
Primary Question
MHE. SILVERY L. SALVATORY aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza Mradi wa Maji Bonde la Lujamate –Buhingo ambao umesimama kwa muda mrefu?
Supplementary Question 3
MHE. BAKARI B. SHINGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo langu la Ukonga kuna Mradi wa Yangeyange, ambao ni mategemeo makubwa kwa wananchi wa Kata ya Pugu, Buyuni, Chanika na Zingiziwa, na pia ni mradi ambao unaonekana umekamilika, lakini hatujawahi kunufaika nao kwa sababu mara nyingi unaripotiwa kuwa na breakdown. Ninaomba nitambue shida ni viwango vya mabomba vilivyotumika pale viko chini, ama utalaamu ni mdogo, ama ni nini? Maana nilikuwa ziarani hata jana, bado tuna shida na tulikuwa tunaambiwa mradi ule una tatizo. Ninaomba nipate ufafanuzi. (Makofi)
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza sana Mheshimiwa Bakari, kwa muda mfupi amekaa jimboni kwake, lakini ameshabaini baadhi ya changamoto hasa zinazolenga akina mama. Sisi kama Serikali tutaendelea kufanya kazi na Waheshimiwa Wabunge ili kuendelea kutatua changamoto za wananchi wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kupokea changamoto hii, na pia ninamwelekeza Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji atume timu iende kuukagua mradi huo, ije na tathmini ya nini kimefanyika, na wapi kuna tatizo? Kama kuna tatizo katika utekelezaji wa mradi, tuchukue hatua kulingana na changamoto ambazo zitabainika baada ya timu hiyo kufanya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapo ninakuhakikishia kwamba tutampatia jibu Mheshimiwa Mbunge kulingana na taarifa itakayopatikana.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved