Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 6 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 94 | 2026-02-03 |
Name
Silvery Luboja Salvatory
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Misungwi
Primary Question
MHE. SILVERY L. SALVATORY aliuliza:-
Je, lini Serikali itaanza Mradi wa Maji Bonde la Lujamate –Buhingo ambao umesimama kwa muda mrefu?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Silvery Luboja Salvatory, Mbunge wa Jimbo la Misungwi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi wa Maji wa Ilujamate – Buhingo uliopo Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza unahusisha ujenzi wa matanki matatu yenye uwezo wa kuhifadhi maji lita 800,000, ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 67, sambamba na ujenzi wa vituo 60 vya kuchotea maji. Utekelezaji wa Mradi huo umefikia wastani wa 40% na unalenga kunufaisha zaidi ya wananchi 84,000 waishio kwenye vijiji 16 vya Wilaya ya Misungwi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, dhamira ya Serikali ni kuhakikisha miradi hiyo inayotekelezwa kwa kupelekewa fedha kadiri zinavyopatikana katika mwaka huu wa fedha 2025/2026 ili ikamilike na kuanza kutoa huduma iliyokusudiwa ukiwemo Mradi wa Maji Ilujamate – Buhingo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved