Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 94 2026-02-03

Name

Silvery Luboja Salvatory

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Primary Question

MHE. SILVERY L. SALVATORY aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza Mradi wa Maji Bonde la Lujamate –Buhingo ambao umesimama kwa muda mrefu?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Silvery Luboja Salvatory, Mbunge wa Jimbo la Misungwi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi wa Maji wa Ilujamate – Buhingo uliopo Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza unahusisha ujenzi wa matanki matatu yenye uwezo wa kuhifadhi maji lita 800,000, ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 67, sambamba na ujenzi wa vituo 60 vya kuchotea maji. Utekelezaji wa Mradi huo umefikia wastani wa 40% na unalenga kunufaisha zaidi ya wananchi 84,000 waishio kwenye vijiji 16 vya Wilaya ya Misungwi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, dhamira ya Serikali ni kuhakikisha miradi hiyo inayotekelezwa kwa kupelekewa fedha kadiri zinavyopatikana katika mwaka huu wa fedha 2025/2026 ili ikamilike na kuanza kutoa huduma iliyokusudiwa ukiwemo Mradi wa Maji Ilujamate – Buhingo.