Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mariam Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa kipande cha barabara kutoka Tosamaganga hadi Igwachanya kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niweze kuuliza swali la nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa changamoto ya wananchi wa Kalenga ni ukamilishwaji wa barabara hiyo. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuhakikisha wanatafuta mpango wa muda ili barabara hiyo iweze kupitika na wananchi wa Kalenga waweze kufanya shughuli zao za kiuchumi kwa vizuri zaidi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Changamoto inayowakuta Kalenga inalikuta pia Jimbo la Temeke katika eneo la Buza, barabara ya kutoka kwa Mama Kibonge, Mashine ya Maji mpaka Azimio. Barabara hiyo imekuwa ni changamoto, kwani unafika mahali magari hayapiti, wananchi wanashindwa kwenda hata kwenye kituo cha afya.

Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuhakikisha wanatengeneza utaratibu wa muda ili barabara hiyo ipitike, wananchi waendelee na shughuli za kiuchumi wakati tukimsubiri mkandarasi aingie na kutengeneza barabara hiyo? (Makofi)

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, ukamilishwaji wa kipande cha barabara kilichobaki cha kilometa 0.9 unakwenda kufanyika kwenye mwaka huu wa fedha 2025/2026, na Serikali ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imetenga fedha, shilingi milioni 829 kwa ajili ya kazi hiyo na ujenzi utakwenda kuanza mara moja, kwa sababu fedha hiyo ipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili la nyongeza ambalo limegusa Wilaya ya Temeke, ndani ya Mkoa wa Dar es Salaam na kwenye wilaya zote tano za Mkoa wa Dar es Salaam, Serikali ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inatekeleza Mradi wa DMDP2. Imetenga milioni 438 Dola za Kimarekani kwa ajili ya kuendeleza miundombinu yote ya msingi ikiwemo barabara aliyoitaja ndani ya Wilaya hiyo ya Temeke, na hivi sasa tuko kwenye hatua mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zipo barabara ambazo tumeshawapa wakandarasi waendelee na kazi na zipo barabara ambazo tunaendelea na usanifu kwa ajili ya kutangaza zabuni na kuanza kazi mara moja.

Name

Timoth Geofrey Anyosisye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa kipande cha barabara kutoka Tosamaganga hadi Igwachanya kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. TIMOTH G. ANYOSISYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi, Jimbo la Kawe changamoto yetu kubwa ni miundombinu ya barabara. Barabara ya Ukwamani - Kwa Mapupu - Kanisani KKKT, Kata ya Kawe, lakini pia barabara ya Kwa Shokoronda na Mongela inayounganisha kata mbili; Kata ya Makongo na Mbezi Juu, na pia barabara inayotoka Bunju A inayopita Kata ya Mabwepande pamoja na Bunju ambayo inaenda hadi Kata ya Wazo pamoja na Kata ya Goba zimekuwepo kwenye mpango wa kujengwa muda mrefu, lakini zimekuwa zikiahirishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wanakawe wanataka kujua je, ni lini barabara hizi zitajengwa? (Makofi)

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO): Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara zote ndani ya Mkoa wa Dar es Salaam likiwemo Jimbo la Kawe, barabara za Mheshimiwa Timoth ambazo ameziongelea miundombinu yote hii tutaitekeleza chini ya Mradi wa DMDP2. Tulianza na DMDP1 tukajenga barabara nyingi sana, na hivi sasa tunakwenda kujenga mtandao wa barabara wa karibia kilometa 257 chini ya Mradi huu wa DMDP2 na barabara hizo anazotaja kwa hakika zitafikiwa.