Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 92 2026-02-03

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa kipande cha barabara kutoka Tosamaganga hadi Igwachanya kwa kiwango cha lami?

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jackson Gedion Kiswaga, Mbunge wa Kalenga, ambalo limeulizwa na Mbunge wa Temeke, Mheshimiwa Mariam Kisangi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Tosamaganga – Igwachanya ni moja kati ya barabara muhimu inayounganisha barabara kuu ya TANZAM na barabara ya Mkoa ya Iringa hadi Msembe yenye urefu wa kilometa 11. Mpaka sasa jumla ya kilometa 10.1 zimeshajengwa kwa kiwango cha lami na kilometa 0.9 iliyosalia inatarajia kujengwa katika mwaka 2025/2026 kupitia Wizara ya Ujenzi chini ya usimamizi wa TANROADS.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, mkandarasi atakayetekeleza kazi hiyo ni Plan Engineering Company na mradi utatekelezwa kwa gharama ya shilingi milioni 829.88.