Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Agnesta Lambert Kaiza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNESTA L. KAIZA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata ya Buguruni?

Supplementary Question 1

MHE. AGNESTA L. KAIZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Katika swali langu la msingi, niliuliza suala zima la ujenzi wa kituo ndani ya Kata ya Buguruni, lakini kwa masikitiko makubwa naona Serikali imejikita kunijibu kuhusiana na ujenzi wa Kituo cha Afya ndani ya Kata ya Kisukuru. Pamoja na yote, ninalo swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Kata ya Buguruni ni kitovu cha uchumi ndani ya Jimbo la Segerea, na kwa sababu hiyo kuna mwingiliano wa watu wengi ukiachilia mbali na hao wakazi 47 plus, jambo linaloonyesha wingi wa wananchi au wanaodumu ndani ya ile kata kwamba ni wengi zaidi ya 47,000 ambayo Serikali imetaja, sasa kwa umuhimu, ningependa kufahamu kwa uhakika kabisa, Serikali imetenga kiasi cha shilingi ngapi kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya ndani ya Kata Buguruni, na ni lini hasa ujenzi huo utaanza? Ahsante.

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali nyongeza la Mheshimiwa Agnesta Lambert Kaiza, Mbunge wa Segerea, kama ifuatavyo: Tayari Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imetenga jumla ya shilingi bilioni nne, kwa maana ya; kwanza, kulipa fidia na kuongeza eneo; pia kuanza ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kisukuru kilichoko ndani ya Kata ya Buguruni.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. AGNESTA L. KAIZA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata ya Buguruni?

Supplementary Question 2

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujua hatima yake, hapa sasa itafika wakati wananchi watawaogopa kwenye mambo haya. Vituo vya mkakati vya afya vinavyojengwa na Serikali, maana yake mlisema mtapeleka shilingi milioni 250 na baadaye shilingi milioni 250 nyingine zitafuata. Sasa kama Kituo cha Mkakati cha Mihingo kinajengwa kwa shilingi milioni 250 na Serikali, halafu tukapata majibu kwamba sasa halmashauri itenge fedha ya kujenga hayo majengo. Sasa hapa kuna mchanganyiko, tunataka tuelewe lipi? Serikali Kuu ndiyo itajenga hivyo vituo kwa maana iliahidi kutoa hiyo shilingi milioni 250 kwa milioni 250; au imeahirisha tena, Mkurugenzi ndio atoe fedha?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni Bunge lako Tukufu lilipitisha kujenga vituo vya kimkakati katika majimbo yote nchini. Tayari tumeshapeleka shilingi bilioni 30 kujenga vituo vya afya vya kimkakati katika majimbo 120 na tayari tumeshaomba fedha nyingine kwa ajili ya kujenga vituo vya afya hivi katika majimbo mengine 94 na yale mengine mapya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ya kwamba tayari tumezielekeza halmashauri kuendelea kujenga majengo ya kutoa huduma katika hospitali hizi zote, lakini kama haitoshi, tutaendelea kuainisha halmashauri zile zenye uwezo na zile ambazo hazina uwezo ili tuweze kutoa fedha Serikali Kuu.

Name

Dr. Wilson Charles Mahera

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Primary Question

MHE. AGNESTA L. KAIZA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata ya Buguruni?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. WILSON C. MAHERA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Butiama ina kata 18, lakini kati ya hizo, kata tisa tu ndiyo zenye vituo vya afya. Pia kuna kata kubwa kama vile Buruma, Buiregi, Bumangi, hazina vituo vya afya. Je, Serikali ina mpango gani kujenga kituo cha afya angalau kwenye kata ya Buruma yenye vijiji sita?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, Serikali inapongeza kwa maana ya kwamba tayari ana vituo tisa ndani ya kata 18, wakati huo kuna baadhi ya kata 14 ina vituo viwili. Kwa hiyo, ni juhudi kubwa ambayo imefanyika na tunaendelea kushirikia na Mheshimiwa Mbunge kuona ya kwamba tunazidi kuongeza vituo vya afya katika jimbo hilo.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNESTA L. KAIZA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata ya Buguruni?

Supplementary Question 4

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Mbali na mpango wa Serikali wa kujenga vituo vya afya na hospitali, mmekuwa na mpango wa ukarabati wa hospitali ambazo zimechakaa. Hospitali ya Manyamanyama iliyopo kwenye Jimbo la Bunda Mjini ni hospitali ambayo majengo yake ni chakavu sana na inatoa huduma katika wilaya za jirani. Ni lini sasa mtatukarabatia Hospitali ya Manyamanyama?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, katika zile fedha ambazo Serikali ilitenga shilingi bilioni 102.08 za ukarabati wa hospitali hizi na hospitali hii aliyoiainisha Mheshimiwa Mbunge imo katika ukarabati huo. (Makofi)

Name

Emmanuel John Khambay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. AGNESTA L. KAIZA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata ya Buguruni?

Supplementary Question 5

MHE. EMMANUEL J. KHAMBAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kituo cha Afya cha Nangara kimejengwa na nguvu za wananchi na ni jengo moja tu la OPD. Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa fedha nyingine ili kuweza kumalizia majengo mengine ili wananchi hao ambao wanafuata huduma umbali mrefu waweze kupata huduma?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, kituo hiki cha afya, kwanza tunawashukuru sana wananchi kwa kutoa nguvu zao na kuweza kuunga mkono juhudi za Serikali, lakini pia nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba nimeshaongea na Mkurugenzi, na kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI niendelee kumwelekeza Mkurugenzi kutenga fedha za ndani ili kukamilisha baadhi ya majengo katika kituo hiki baada ya kutoa OPD waendelee kutoa na huduma nyingine ambazo zinatakiwa kwenye kituo cha afya. (Makofi)

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. AGNESTA L. KAIZA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata ya Buguruni?

Supplementary Question 6

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Mchinga halina hospitali hata moja, na lina vituo vya afya viwili. Kwa kuwa jimbo hili halina hospitali, je, ni lini Kituo cha Afya cha Kitomanga kitapandishwa hadhi ya kuwa hospitali, na kwa sababu mchakato wake wa kupandishwa hadhi ni wa muda mrefu, nilikuwa ninaomba majibu ya Serikal, lini kituo hiki kitapandishwa hadhi na kuwa hospitali?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mama Salma kwa kufuatilia afya za wananchi wake katika Jimbo la Mchinga. Pili, tayari tumeshachukua maombi ya kupandisha Kituo cha Afya Kitomanga kuwa hospitali ili kiweze kutoa huduma katika eneo kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeshakaa na wataalamu, na nimhakikishie Mheshimiwa Mama Salma Kikwete kwamba ndani ya muda mfupi tathmini itatoka na kuanza ujenzi na kukipandisha kituo hiki kuwa hospitali. (Makofi)