Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 91 2026-02-03

Name

Agnesta Lambert Kaiza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNESTA L. KAIZA aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata ya Buguruni?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Agnesta Lambert Kaiza, Mbunge wa Segerea, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuboresha huduma za afya ngazi ya msingi kwa kujenga vituo vya afya kwenye kata za kimkakati. Buguruni ni miongoni mwa kata zilizopo Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam yenye wakazi wapatao 47,278. Kwa sasa hii wanapata huduma za afya katika Kituo cha Afya cha Buguruni na Zahanati ya Bungoni umbali usiozidi kilometa mbili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka 2023/2024 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ilifanya uthamini na kulipa fidia nyumba tatu kiasi cha shilingi milioni 245 kwenye eneo lenye ukubwa wa takribani mita za mraba 900 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, eneo hilo halitoshelezi ambapo mwaka 2026/2027 Serikali kupitia Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imefanya tathmini na kulipa fidia takribani nyumba saba ili kuongeza ukubwa wa eneo kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Buguruni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka 2025/2026 Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imetenga jumla ya shilingi bilioni nne kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya katika Kata ya Kisuru. Ujenzi huu ni wa ghorofa na Halmashauri ya Jiji ipo katika maandalizi na utaratibu wa manunuzi ya kumpata mzabuni. (Makofi)