Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kupeleka gari la kubebea wagonjwa katika Kituo cha Afya cha Nyakahura Wilayani Biharamulo?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali. Ninakiri kwamba tulipokea gari moja la wagonjwa, na gari moja la usimamizi, kama alivyosema kwenye jibu la msingi Tunaishukuru sana Serikali. Hata hivyo kwa jiografia ya Biharamulo, Wilaya ile ni kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapoongelea Kituo cha Afya cha Nyakahura ni kilometa 82 kutoka Biharamulo Mjini, lakini Waziri Mkuu akiwa katika ziara Mkoa wa Kagera tarehe 21/09/2021 specifically alitoa ahadi ya ambulance kwa Kata ya Nyakahura kwa ajili ya hicho kituo cha afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ningependa kujua ahadi hiyo ya Waziri Mkuu ninayoiongelea ndiyo inayoelekea Nyakahura pale? Kwa hiyo, swali la kwanza, kwa sababu ni ahadi ya Waziri Mkuu, ni lini tutapa ile ambulance sawa na Waziri Mkuu alivyokuwa ameahidi kwa ajili ya wananchi wa Nyakahura? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Kata ya Kabindi ni center kubwa sana ambayo inahudumia Kata karibu tano ukielekea njia ya Mwanza ambazo nyingine zinapatikana zaidi ya kilometa 70 mpaka 80 kutoka Biharamulo Mjini na center ile ni kubwa, lakini upande ule hatuna kabisa ambulance ambayo inaweza ikakaa pale kwa ajili ya kuhudumia hizo Kata tano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, pamoja na hii ya Nyakahura, ni lini sasa tutapata ambulance nyingine itakayokuwa inakaa Kabindi kwa ajili ya kuhudumia kata tano inapotokea dharura aidha waletwe Biharamulo Mjini au wapelekwe Mwanza kwa ajili ya kwenda kupata matibabu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kupata pia majibu ya Serikali kuhusu issue hiyo ya ambulance nyingine ya pili. (Makofi)

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli ninakiri na kwenye kampeni nilifika katika Jimbo la Biharamulo Magharibi na anayoyazungumza Mheshimiwa Chiwelesa yako sahihi. Nimhakikishie ahadi za viongozi wetu wakuu wote nchini zinakwenda kutekelezwa kwa wakati, na tumeshaomba ambulance nyingine, zinakuja kutoka Wizara ya Afya. Zikifika tunakwenda kutekeleza ahadi hii ya Mheshimiwa Waziri Mkuu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi la pili, tunalichukua kama Serikali ili kuangalia kulingana na idadi za ambulance tutakazokuwa tunazipata ili kuweza kuwaongezea. Ni kweli Jimbo hili kijiografia ni pana na lina idadi kubwa ya watu. (Makofi)

Name

Arif Suleiman Premji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kupeleka gari la kubebea wagonjwa katika Kituo cha Afya cha Nyakahura Wilayani Biharamulo?

Supplementary Question 2

MHE. ARIF S. PREMJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Je, ni lini Serikali itapeleka gari la kubebea wagonjwa Kituo cha Afya Kilambo, Mtwara DC ukizingatia kituo hicho kipo mpakani mwa Msumbiji? (Makofi)

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu magari ya kubebea wagonjwa, tuna maeneo yenye upungufu kweli, tunakiri, na tumeendelea kuyaomba magari haya pamoja na yale mengine ambayo tayari Serikali imeshayatoa katika Halmashauri zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, ombi lake tunalichukua kwa maana ya kwamba tunapoenda kuomba magari mengine na yeye awe mnufaika katika gari hili la ambulance. (Makofi)

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kupeleka gari la kubebea wagonjwa katika Kituo cha Afya cha Nyakahura Wilayani Biharamulo?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kumwuliza Mheshimiwa Waziri, Halmashauri ya Wilaya ya Geita ina Majimbo matatu na ina hospitali mbili zenye hadhi ya Wilaya kikiwemo na kituo kikubwa cha afya kilichopo Nyarugusu kwenye Jimbo lake Mheshimiwa Waziri na magari tunayo mawili tu. Anapopatikana mgonjwa kutoka Nyarugusu inalazimika kutoa gari kilometa 100 kwenye Hospitali ya Wilaya Nzera au kilometa 80 kule Katoro. Je, ni lini Serikali itapeleka ambulance kwenye kituo kikubwa cha Nyarugusu? (Makofi)

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niwape pole na kuwapongeza wananchi wa Jimbo la Busanda, Majimbo yote matatu yaliyo katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita DC kwanza kwa uvumilivu mkubwa na usikivu mkubwa na wanatuunga mkono viongozi wao. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Kasheku Musukuma, tutafanya namna ya kupeleka gari la ambulance ili kuokoa maisha ya wagonjwa wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tuendelee kusubiri, Serikali tumeshaomba magari haya kutoka Wizara ya Afya. Hivyo, Jimbo la Busanda na lenyewe ni wanufaika katika kupata ambulance mpya. (Makofi)

Name

Regina Henry Mikenze

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kupeleka gari la kubebea wagonjwa katika Kituo cha Afya cha Nyakahura Wilayani Biharamulo?

Supplementary Question 4

MHE. REGINA H. MIKENZE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami ninapenda kuuliza swali. Ni lini Kituo cha Afya cha Kata ya Rwamgasa kitakamilishwa na kuanza kutoa huduma? (Makofi)

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, nilifika katika Kituo cha Afya cha Rwamgasa na kiukweli kimeanza kutoa huduma za OPD na kuna majengo yanazidi kuongezwa pale kupitia mbia wetu wa Buckreef, na majengo haya yanakwenda kukamilika ndani ya mwezi wa tatu na kuanza kutoa huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeshatoa maelekezo mahususi kwa Mkurugenzi kufuatilia kwa ukaribu katika ujenzi wa majengo haya ili akina mama wetu wanaojifungua zaidi ya 200 mpaka 250 kwa mwezi waweze kupata huduma hii ya afya ya msingi. (Makofi)