Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 6 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 90 | 2026-02-03 |
Name
Eng. Ezra John Chiwelesa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Biharamulo Magharibi
Primary Question
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: -
Je, lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kupeleka gari la kubebea wagonjwa katika Kituo cha Afya cha Nyakahura Wilayani Biharamulo?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Ezra John Chiwelesa, Mbunge wa Jimbo la Biharamulo Magharibi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika kipindi cha mwaka 2021/2022 hadi 2024/2025 imenunua jumla ya magari 594 zikiwemo ambulance 382 na magari ya usimamizi ufuatiliaji 212 katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kote nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo imepokea gari moja la kubebea wagonjwa mwezi Novemba, 2023 na kupelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Biharamulo. Aidha, idadi hii inafanya Halmashauri ya Biharamulo kuwa na jumla ya magari matatu ya kubebea wagonjwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya ununuzi wa magari ya wagonjwa kwa awamu kwa ajili ya vituo vya afya vyenye uhitaji kote nchini kikiwemo Kituo cha Afya Nyakahura. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved