Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Devotha Daniel Mburarugaba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DEVOTHA D. MBURARUGABA aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kurekebisha kigezo kinachowapunguzia fursa wanafunzi wa shule binafsi kupata mikopo ya elimu ya juu?
Supplementary Question 1
MHE. DEVOTHA D. MBURARUGAMBA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimshukuru Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya kwenye sekta ya elimu. Pia naomba nimpongeze Naibu Waziri kwa kazi kubwa anayoifanya. Nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza. Je, ni lini Serikali itaondoa vigezo hivi ili kuweza kuweka usawa kwa shule hizi za sekta binafsi, kwani tunafahamu kabisa kwamba wanafunzi hawa wanaosoma sekta binafsi wanasaidiwa na wazazi ambao wanajikwamua kwenye kipato cha chini, yaani wanajinyima, pia wanasaidiwa na marafiki, ndugu, jamaa na watu mbalimbali kutoa misaada hii?
Mheshimiwa Spika, swali la pili. Je, ni lini Serikali itaondoa vigezo hivi ili kuwatia moyo wazazi hawa ambao wameweza kujinyima kuwalipia ada na watu mbalimbali wanaochangia hizi ada, ili kupunguza msongamano kwenye shule za umma kwa maana ya shule za Serikali? Ahsante. (Makofi)
Name
Wanu Hafidh Ameir
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, mwongozo wa utoaji wa mikopo ya elimu ya juu hauhitaji kigezo cha aina ya shule aliyosoma mwombaji, iwe ya Serikali ama iwe ya binafsi. Hivyo, wanafunzi wote sifa za kupata mkopo wa elimu ya juu hupatiwa mkopo huo kwa mujibu wa utaratibu wa vigezo vilivyowekwa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ni kwamba, Sheria ya Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Sura 178, imeweka vigezo mahsusi ambavyo mwanafunzi mlengwa hutakiwa awe navyo. Vigezo hivyo ni pamoja na; awe Mtanzania mhitaji, awe amepata udahili katika taasisi zinazotambulika, pia awe amejaza fomu hizo kwa usahihi.
Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza kwenye jibu langu la msingi na swali la nyongeza, ni kwamba hakuna kigezo kinachowapunguzia fursa wanafunzi wa shule binafsi kupata mikopo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved