Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 2 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 26 2026-01-28

Name

Devotha Daniel Mburarugaba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEVOTHA D. MBURARUGABA aliuliza:-

Je, Serikali haioni umuhimu wa kurekebisha kigezo kinachowapunguzia fursa wanafunzi wa shule binafsi kupata mikopo ya elimu ya juu?

Name

Wanu Hafidh Ameir

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa ruhusa yako naomba nijibu swali la Mheshimiwa Devotha Daniel, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, upangaji na utoaji mikopo ya elimu ya juu unaongozwa na Sheria ya Bodi ya Mikopo (Sura 178) ambayo inabainisha sifa za msingi za mwombaji, zikiwepo sifa za kitaaluma za kujiunga na taasisi za elimu ya juu kwa waombaji waliothibitika kutokuwa na uwezo wa kumudu gharama za elimu ya juu.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutoa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu wanaotoka katika kaya maskini bila kujali mwombaji ametoka shule za Serikali au shule binafsi. Kwa msingi huo, Serikali kupitia Bodi ya Mikopo imeweka utaratibu wa kuzingatiwa kwa waombaji wote, bila kujali shule aliyosoma ilimradi mwombaji amekidhi vigezo vilivyowekwa ikiwemo ujazaji wa taarifa sahihi.