Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 2 | Education, Science,Technology and Vocational Training, | Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia | 26 | 2026-01-28 |
Name
Devotha Daniel Mburarugaba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DEVOTHA D. MBURARUGABA aliuliza:-
Je, Serikali haioni umuhimu wa kurekebisha kigezo kinachowapunguzia fursa wanafunzi wa shule binafsi kupata mikopo ya elimu ya juu?
Name
Wanu Hafidh Ameir
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa ruhusa yako naomba nijibu swali la Mheshimiwa Devotha Daniel, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, upangaji na utoaji mikopo ya elimu ya juu unaongozwa na Sheria ya Bodi ya Mikopo (Sura 178) ambayo inabainisha sifa za msingi za mwombaji, zikiwepo sifa za kitaaluma za kujiunga na taasisi za elimu ya juu kwa waombaji waliothibitika kutokuwa na uwezo wa kumudu gharama za elimu ya juu.
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutoa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu wanaotoka katika kaya maskini bila kujali mwombaji ametoka shule za Serikali au shule binafsi. Kwa msingi huo, Serikali kupitia Bodi ya Mikopo imeweka utaratibu wa kuzingatiwa kwa waombaji wote, bila kujali shule aliyosoma ilimradi mwombaji amekidhi vigezo vilivyowekwa ikiwemo ujazaji wa taarifa sahihi.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved