Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Chacha Mwita Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. ENG. CHACHA M. WAMBURA aliuliza:- Je, hatua gani zimefikiwa katika kuandaa mpango wa kuendeleza na kukamilisha ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu - Manispaa ya Geita?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. CHACHA M. WAMBURA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Naibu Waziri amesema kwamba mapitio yanaendelea. Ninaomba kufahamu kwamba je, Serikali haioni haja ya kufanya mapitio haya kwa haraka ili basi uwanja ule uweze kukamilika na ikiwezekana ukamilike kabla ya mwakani ambapo tunaenda kuwa na mashindano ya AFCON ambayo yataenda kufanyika katika nchi zetu tatu za Afrika Mashariki na ambapo tunaamini Geita ni centre ya Kenya, Tanzania na Uganda?
Mheshimiwa Spika, kama tutaweza kukamilisha uwanja huu kwa wakati basi zile timu zinaweza zikafanya mazoezi au kutumia vile viwanja wakati wa mashindano.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Serikali katika sehemu nyingine tumekuwa tukishirikiana na tukifanya vizuri sana, na tunavyoshirikiana na private sector, je, katika suala hili la viwanja hapa Tanzania, Serikali haioni sasa ni wakati sahihi ya ku-engage private sector ili kushirikiana nao na kuwa-support ili tuweze kupata viwanja vingi zaidi ili tuendeleze michezo?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Chacha Mwita Wambura kwa kufuatilia ujenzi wa uwanja huu. Pia ninaupongeza uongozi wa Mkoa wa Geita kwa kuwa karibu na wawekezaji hawa hadi kufikia kuweka fedha hizi kwa ajili ya ujenzi.

Mheshimiwa Spika, baada ya kumpata mkandarasi mshauri, tayari kiasi cha fedha cha shilingi bilioni 3.4 zimetengwa kwa ajili ya ukamilishaji wa jukwaa juu, majukwaa ya watazamaji na sehemu ya kuchezea mpira (pitch) ambapo inakadiriwa kuwa ujenzi utakamilika ifikapo Oktoba, 2026.

Mheshimiwa Spika, kulingana na idadi ya wakazi wa Mkoa wa Geita inayokadiriwa kufikia milioni tatu kutokana na sensa ya watu na makazi iliyofanyika mwaka 2022, uwanja huu Serikali inauona kama ni sehemu ya kuleta tabasamu kwa Watanzania walioko katika Mkoa wetu wa Geita.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kumwahisha mkandarasi kuweza kukamilisha ujenzi wa uwanja huu, tunao uhakika kabisa kwamba uwanja huu wenzetu wa Wizara ya Michezo wanaweza wakauona kama ni sehemu ya AFCON ya mwaka huu kama utakamilika kwa wakati.
Mheshimiwa Spika, Serikali inamhakikishia Mheshimiwa Mwita kuendelea kufuatilia kwa ukaribu ili kuhakikisha uwanja huu unaweza kutoa huduma hii ya michezo.

Name

Mabula Johnson Magangila

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. ENG. CHACHA M. WAMBURA aliuliza:- Je, hatua gani zimefikiwa katika kuandaa mpango wa kuendeleza na kukamilisha ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu - Manispaa ya Geita?

Supplementary Question 2

MHE. MABULA J. MAGANGILA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi hii, naomba kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, je, ni mpango upi wa Serikali wa kujenga kiwanja kikubwa cha kisasa katika Mji wa Kahama ambao unakua kwa kasi sana sasa hivi?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na mipango hii ya kuhakikisha vile viwanja ambavyo vipo chini ya Halmashauri vinajengwa kulingana na vipaumbele vya Halmashauri na jinsi wataalam wetu wanavyoweza kuibua miradi katika maeneo yao. Kama kitakuwa kipo ndani ya Halmashauri kiwanja hicho, tutaweza kuhakikisha kinajengwa kwa wakati, na kama kipo kwa wenzetu Wizara ya Michezo wataweza kutolea majibu katika swali hilo.