Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 24 2026-01-28

Name

Chacha Mwita Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. ENG. CHACHA M. WAMBURA aliuliza:-

Je, hatua gani zimefikiwa katika kuandaa mpango wa kuendeleza na kukamilisha ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu - Manispaa ya Geita?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): alijibu:-

Mheshimiwa Spika, uwanja wa mpira wa miguu - Geita ulianza kujengwa mwaka 2021 kwa kutumia fedha za uwajibikaji wa kijamii wa mashirika (CSR) kwa gharama ya shilingi bilioni 5.46 kupitia mgodi wa Geita Gold Mine. Hata hivyo, ujenzi ulisimama mwaka 2023 ukiwa 71%, baada ya Mkandarasi EFQ Co. Ltd kusitishiwa mkataba kutokana na mabadiliko ya kanuni ya miradi ya CSR.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na mgodi wa Geita Mine Ltd imepata mkandarasi mshauri NORPLAN ambaye amefanya mapitio ya gharama halisi za kukamilisha ujenzi wa uwanja huo na kiasi cha shilingi bilioni tano zinahitajika. Aidha, Serikali inaendelea na mapitio ya gharama zilizowasilishwa na mkandarasi mshauri ili kuweza kuendelea na ujenzi kupitia fedha za CSR zitakazotengwa katika mwaka 2026/2027.