Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
George Natany Malima
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mpwapwa
Primary Question
MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa kituo cha afya Kata ya Iwondo ili wananchi waanze kupata huduma?
Supplementary Question 1
MHE. GEORGE N. MALIMA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina swali moja la nyongeza. Kwa kuwa, Waziri na Naibu Waziri katika Wizara hii wote ni wageni natamani sana wapate fursa ya kufika kuona ujenzi unavyoendelea. Je, ni lini Waziri ataandamana nami kufika katika Kituo cha Iwondo cha Afya, ili aweze kuona ujenzi unavyoondelea pale?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa George Natany Malima. Sisi Wizara tunafanyakazi ya kuzitembelea halmashauri zote nchini na tumekwishaanza zoezi hilo. Namhakikishia tu Mheshimiwa Natany Malima, baada ya Bunge hili tunaweza kuongozana kwenda Jimbo la Mpwapwa katika halmashauri hii na kukitembelea kituo hiki. (Makofi)
Name
Ester Amos Bulaya
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa kituo cha afya Kata ya Iwondo ili wananchi waanze kupata huduma?
Supplementary Question 2
MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi nami niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Halmashauri ya Mji wa Bunda tunajenga hospitali yetu ambayo iko Kata ya Bunda Stoo. Serikali imetupatia fedha, lakini tangu mwaka juzi, 2024, kuna shilingi milioni 800 zilirudi na hazijarudishwa bado, huo mradi umesimama. Ni lini mtaturudishia fedha zetu shilingi milioni 800 tuweze kukamilisha hospitali ya Wilaya ambayo ina mchango mkubwa kwenye Jimbo la Bunda Mjini? (Makofi)
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, Serikali imejipambanua katika kuhakikisha huduma za afya zinawafikia wananchi wote. Nawahakikishia wananchi wa Jimbo la Bunda, fedha zao zipo na tutazielekeza kuendelea na shughuli ambazo Serikali ilikuwa imezielekeza. (Makofi)
Name
Khalid Mussa Nsekela
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kyerwa
Primary Question
MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa kituo cha afya Kata ya Iwondo ili wananchi waanze kupata huduma?
Supplementary Question 3
MHE. KHALID M. NSEKELA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi ya kuuliza swali hili la nyongeza. Kwanza naishukuru Serikali sikivu ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia wahudumu 58 katika dirisha hili la ajira za afya kwa Wilaya ya Kyerwa.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, Kituo cha Afya cha Nkwenda ni kikubwa na kinatoa huduma zaidi ya Kata 19 na sometime kinatoa huduma nje ya Wilaya ya Kyerwa, lakini kituo hiki hakina gari ya uhakika ya wagonjwa (ambulance), je, ni lini Serikali itatupatia gari la uhakika kwa ajili ya kutoa huduma safi kwa kituo hicho? Ahsante.
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT.JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, tunakumbuka sote humu ndani katika kipindi cha miaka mitano Serikali imenunua jumla ya magari ya kubebea wagonjwa 316, pamoja na magari ya wakaguzi 212 na ambulance za awamu ya kwanza tumeshazigawa katika Halmashauri ambazo ziliainishwa. Nimhakikishie kuwa, awamu ya pili kituo hiki kitakuwa wanufaika wa gari la ambulance.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved