Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Dr. Yahaya Esmail Nawanda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nanyumbu
Primary Question
MHE. DKT. YAHYA E. NAWANDA aliuliza:- Je, lini Stendi ya Mabasi ya Mji wa Kitangari, Newala, itajengwa?
Supplementary Question 1
MHE. DKT. YAHYA E. NAWANDA: Mheshimiwa Spika, naomba kuuliza Serikali maswali mawili ya nyongeza. Swali langu la kwanza, je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara zote zilizopo katika Mji wa Kitangari? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili. Je, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara za lami kutoka katika Kijiji cha Maputi hadi Ndanda, na pia, katika Kijiji cha Chiwonga, Pacha Nne, hadi Nanganga? Ahsante. (Makofi)
Name
Kwagilwa Reuben Nhamanilo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Handeni Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO): Mheshimiwa Spika, Serikali tayari imeshaanza kujenga barabara zilizopo katika Mji wa Kitangari. Tumeanza na barabara ya kutoka kwa Mzee Lada mpaka kwa Mzee Twalibu, ambayo ina urefu wa kilomita moja, na siyo tu kwamba tumeishia kuijenga, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan amehakikisha barabara hiyo imewekewa taa pia, na inatumika.
Mheshimiwa Spika, kadiri fedha zitakavyoendelea kupatikana tutaendelea na ujenzi wa barabara za mji huo. Barabara ya kutoka Msikiti Mkubwa kwenda kituo cha afya karibu na stendi, na vilevile Barabara ya Mnakute hadi Halmashauri na Barabara ya VETA hadi Nachirindima.
Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, Barabara ya Maputi – Ndanda, Chuonga – Pacha Nne kwenda Mkongi hadi Nanganga njia panda ya kwenda Ruangwa, Serikali itatekeleza kama ilivyoahidi kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya 2025/2030. Nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia barabara hizi kwa umakini mkubwa. (Makofi)
Name
Zacharia Paulo Issaay
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbulu Mjini
Primary Question
MHE. DKT. YAHYA E. NAWANDA aliuliza:- Je, lini Stendi ya Mabasi ya Mji wa Kitangari, Newala, itajengwa?
Supplementary Question 2
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Serikali ilikusudia kujenga stendi ya mabasi, soko, dampo na machinjio katika Mji wa Mbulu kwa kupitia Mradi wa TACTIC. Hadi sasa Serikali imefikia hatua gani katika kutekeleza mradi huu?
Name
Kwagilwa Reuben Nhamanilo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Handeni Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO): Mheshimiwa Spika, ujenzi wa stendi katika Mji wa Mbulu ni sehemu ya Miradi ya TACTIC tutakayoitekeleza katika awamu ya tatu. Hivi sasa Serikali inaendelea na ukamilishaji wa Usanifu wa miradi yote 18, kwa maana ya miji yote 18 iliyomo kwenye awamu ya tatu. Mara tu baada ya usanifu kukamilika, taarifa zote tutazikusanya na tutakwenda hatua inayofuata ya kutangaza zabuni kumpata mjenzi, pamoja na mkandarasi mshauri. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved