Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 22 2026-01-28

Name

Dr. Yahaya Esmail Nawanda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. DKT. YAHYA E. NAWANDA aliuliza:-

Je, lini Stendi ya Mabasi ya Mji wa Kitangari, Newala, itajengwa?

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Yahya Esmail Nawanda, Mbunge wa Newala Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Newala ina stendi ya mabasi iliyopo katika Mji wa Kitangari, ambayo imepangwa kutengewa fedha katika Mpango wa Bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027 kupitia mapato ya ndani ya halmashauri. Kutokana na stendi hiyo kutokidhi mahitaji ya sasa ya usafiri, halmashauri imepanga kufanya maboresho ya awali kwa kiwango cha changarawe ili kuboresha utoaji wa huduma za wananchi.

Mheshimiwa Spika, sambamba na maboresho hayo halmashauri imeanza kutafuta eneo mahsusi, kwa ajili ya ujenzi wa stendi ya kisasa itakayokidhi mahitaji ya Mji wa Kitangari na maeneo ya jirani.