Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniventura Destery Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha za kumalizia Mradi wa Maji Lugeye Kigangama uliosimama kwa miaka miwili sasa?

Supplementary Question 1

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali. Ninayo maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa mradi huu umechukua muda mrefu na mkandarasi ameshafanya kazi zaidi ya shilingi bilioni 4.5 na amelipwa shilingi bilioni 1.5, je, nini mkakati wa Serikali wa kupeleka fedha ili huyo mkandarasi arudi kazini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Kwa kuwa kuna miradi ambayo imefikia 98%, Mheshimiwa Naibu Waziri anaifahamu, Mradi wa Iseni, Nyang’hanga, Mradi wa Mwarina – Mwamabanza – Salong’we, lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kumalizia hizo asilimia ambazo zimebaki ili wananchi waweze kupata huduma?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Boniventura Kiswaga, Mbunge mahiri kutoka Mkoa wa Magu katika Jimbo la Magu, kwa kazi nzuri ambayo anaendelea kuifanya ya kuwatetea hasa katika kumtua mama ndoo kichwani ambayo ni falsafa ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nikiri kwamba Mheshimiwa Mbunge ni mfuatiliaji mzuri sana na kwa mantiki hiyo, hivi sasa ninayo maelekezo ya Mheshimiwa Waziri wa Maji Mheshimiwa Jumaa Hamidu Aweso kuhakikisha mradi huu na mkandarasi huyu ndani ya malipo ya mwezi huu tuhakikishe kwamba analipwa. Ndiyo mkakati wa kuhakikisha kwamba tutaendelea kumlipa mpaka pale ambapo fedha zote zitakuwa zimeshalipwa ili mradi uweze kukamilika. Hivi sasa mradi uko 65% na tunaamini kwamba akishalipwa atarudi site.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge, mpaka sasa mkandarasi tumeshamwita hapa Dodoma, leo tutakuwa na mazungumzo naye ili tuhakikishe tutakapolipa hizi fedha, arudi site moja kwa moja ili tukaone sasa matunda ya kazi kubwa inayofanywa na Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayo miradi mingine ndani ya Jimbo la Magu ambapo ni matokeo ya kazi nzuri sana ya Mheshimiwa Mbunge. Tunayo miradi takribani sita, ukiwemo wa Lugeye. Miradi hii kwa jumla yake kuna uwekezaji mkubwa sana wa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zaidi ya shilingi 18,000,000,000 zimewekezwa pale, na pia miradi ya Nyang’hanga, Iseni, Sagani, Misungwi, Mahaha, Nsola, Bubinza yote hiyo iko katika hatua mbalimbali. Mmoja upo 90%, mwingine 98%, mwingine uko 65%, mwingine uko 50%. Tunaamini kwamba tukiendelea kupeleka fedha, miradi hii itatoa matokeo kwa haraka sana. Nakushukuru sana.

Name

Adonis Alfred Bitegeko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha za kumalizia Mradi wa Maji Lugeye Kigangama uliosimama kwa miaka miwili sasa?

Supplementary Question 2

MHE. ADONIS A. BITEGEKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kuniona na kunipa nafasi. Jimbo la Muleba Kaskazini, Wilaya ya Muleba ina miradi miwili ya maji, Mradi wa Makongora na Mradi wa Iroba ambayo kwa muda mrefu inasubiri Serikali kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji. Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo ili kusaidia wananchi takribani 9,000 kupata huduma ya maji salama?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Sera yetu ya Maji, kwanza kabisa ni kuhakikisha kwamba maji yawe safi, yawe salama na yawe ya kutosheleza. Ujenzi wa chujio ni sehemu ya sera kwa sababu ni lazima chujio hilo liweze kutumika katika kuhakikisha kwamba maji yanakuwa safi, na pia yanatibiwa vizuri ili yawafikie wananchi yakiwa salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima chujio hilo liweze kutumika katika kuhakikisha kwamba maji yanakuwa safi na yanatibiwa vizuri ili yawafikie wananchi yakiwa salama. Nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge na kwa kazi kubwa. Ninafahamu ana miezi michache tangu ameingia, lakini amekuwa mfuatiliaji mzuri sana wa miradi hii ya maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi Wizara ya Maji tunaahidi kuendelea kumpa ushirikiano Mheshimiwa Mbunge ili kuhakikisha kwamba fedha zinapelekwa kwa ajili ya kuhakikisha kwamba chujio hili linajengwa ili likamilike na kutoa huduma iliyokusudiwa kwa wananchi. Ninakushukuru sana.

Name

Mecktridis Fratern Mdaku

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha za kumalizia Mradi wa Maji Lugeye Kigangama uliosimama kwa miaka miwili sasa?

Supplementary Question 3

MHE. MECKTRIDIS F. MDAKU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Jimbo la Malinyi lina Miradi ya Maji katika Kijiji cha Misegese – Ihowanja na Mtimbira na miradi hii imekaa muda mrefu zaidi ya miaka mitatu sasa bila kukamilika. Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa fedha ili kukamilisha miradi hii? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana na ninampongeza sana Mheshimiwa Mbunge wa Malinyi, ni Mbunge mahiri, na pia ni Mjumbe katika Kamati yetu ya Maji na Mazingira, tunaendelea kutambua mchango wake mkubwa sana katika kuishauri Serikali na kuisimamia. Katika kuwatetea wananchi wake, sisi tutaendelea kumpa ushirikiano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayo madai ya wakandarasi ndani ya Jimbo lake, na tayari yameshaletwa na yameshafika kwenye Ofisi ya Katibu Mkuu, wanayafanyia kazi. Tunaamini kabisa kwamba ndani ya kipindi cha miezi miwili mitatu hii, tutapeleka fedha ili wakandarasi hawa walipwe ili miradi hii ambayo imekaa kwa muda mrefu iweze kukamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni dhamira ya Serikali, siyo hiyo miradi pekee, miradi yote inayoendelea kutekelezwa nchini tunayo maelekezo mahsusi ya Mheshimiwa Rais kuhakikisha kwamba tunakamilisha kwanza hii miradi ambayo imeishaanza badala ya kuanza miradi mipya ili kuhakikisha kwamba tunaanza kupata matokeo kabla ya kuanzisha miradi mingine mipya. Ninakushukuru sana.

Name

Moses Charles Bujaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha za kumalizia Mradi wa Maji Lugeye Kigangama uliosimama kwa miaka miwili sasa?

Supplementary Question 4

MHE. MOSES C. BUJAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru. Mradi wa Maji wa Ziwa Victoria kuja Mji Mdogo wa Malya umesimama. Swali langu ni kutaka kujua, ni lini mkandarasi atalipwa fedha ili arudi kazini na kukamilisha mradi huu? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Moses Charles Bujaga, Mbunge wa Sumve, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa mradi ule unaopita Hungumalwa – Malya kwenda kule Sumve, na pia mradi huu unaenda mpaka kwa Mheshimiwa Mashimba Ndaki. Mheshimiwa Mbunge tulishakaa pamoja na mkandarasi kwa pamoja tukakubaliana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, ninaomba sasa nimhakikishie kwamba ule mpango wa kuhakikisha kwamba analipwa, tumeweka kipaumbele katika kipindi hiki cha miezi miwili ili mkandarasi aweze kulipwa na arudi site, kwa sababu tunajua kuna matanki ambayo tayari ameshayajenga, lakini kuna kilometa kadhaa za kulaza mabomba ili aweze kumalizia na kuhakikisha kwamba wananchi wa maeneo hayo wanaweza kunufaika na huduma ya majisafi na salama. Ninakushukuru sana.