Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 8 Water and Irrigation Wizara ya Maji 80 2026-04-14

Name

Boniventura Destery Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: -

Je, lini Serikali itatoa fedha za kumalizia Mradi wa Maji Lugeye Kigangama uliosimama kwa miaka miwili sasa?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Boniventura Kiswaga, Mbunge wa Jimbo la Magu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipaumbele cha Serikali ni kuhakikisha miradi yote inayoendelea na utekelezaji, inakamilika na kuanza kutoa huduma iliyokusudiwa kwa wananchi ukiwemo mradi wa Lugeye – Kigangama uliopo Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huo unagharimu zaidi ya shilingi bilioni saba na umefikia wastani wa 65% za utekelezaji ambapo unahusisha ujenzi wa dakio (intake) yenye uwezo wa kuzalisha maji lita milioni 3.7 kwa siku kutoka chanzo cha ziwa Victoria. Ujenzi wa mtambo wa kutibu maji (treatment plant), ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita 1,000,000, ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 52 sanjari na ujenzi wa vituo 10 vya kuchotea maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kupeleka fedha za utekelezaji wa mradi huo kadiri zinavyopatikana ili kuhakikisha unakamilika ndani ya mwaka wa fedha 2026/2027 na kuanza kutoa huduma iliyokusudiwa kwa zaidi ya wananchi 47,076 waishio katika vijiji saba vya Kitongosima, Lugeye, Kigangama, Bundilya, Nyanguge, Bugumangala na Muda.