Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Emmanuel John Khambay
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Mjini
Primary Question
MHE. EMMANUEL J. KHAMBAY aliuliza: - Je, lini Serikali itafanya maboresho ya makazi ya askari pamoja na kununua magari mapya Gereza la Babati Mjini?
Supplementary Question 1
MHE. EMMANUEL J. KHAMBAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali, nina swali moja la nyongeza. Kama ambavyo amekiri mwenyewe kwamba Gereza la Babati ni miongoni mwa magereza yaliyojengwa kwa miaka ya zamani, je, ni nini mpango wa Serikali wa kujenga gereza lingine jipya ambalo pia litakuwa ni gereza la kisasa linaloendana na wakati?
Name
Mohammed Mahmoud Ayoub
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Chaani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamshukuru sana Mheshimiwa Dkt. Emmanuel kwa swali lake la nyongeza ambalo ni la muhimu sana. Kwanza tukiri ni kweli tuna uhitaji mkubwa wa magereza nchini, kwani katika hali ya sasa nchi nzima tuna idadi ya magereza 129. Kati ya magereza hayo, magereza 10 yana hadhi ya magereza ya kanda, magereza 76 yana hadhi ya magereza ya mikoa na wilaya na magereza 43 ni magereza ya wazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hali hiyo, tuna upungufu wa takribani wilaya 50 ambazo hazina magereza, lakini kazi inayoendelea sasa ya ujenzi wa magereza katika maeneo mbalimbali ambayo kwa kweli kwa baadhi ya maeneo imepiga hatua nzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, Wilaya ya Karatu gereza limekamilika, Wilaya ya Kilosa limeanza ujenzi, Wilaya ya Gairo linaendelea, Wilaya ya Kingurungundwa kule Mchinga nalo linaendelea. Ninaamini kwamba na maeneo mengine pia tutaendelea na hatua kama ambavyo nimetaja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa Serikali kwenye ujenzi wa magereza haya ni kuendelea kuweka fedha kwenye bajeti, kwani tayari tumeshafanya tathmini ya uhitaji wa magereza hayo kwamba kila gereza moja linahitaji wastani wa shilingi bilioni nane kulijenga. Hivyo, kwa magereza 50 tunahitaji wastani wa shilingi bilioni 40 ili tuweze kujenga magereza hayo. Sambamba na hilo, tunafahamu pia ipo changamoto kubwa ya makazi ya Askari Magereza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jambo hilo, pia Serikali imeandaa mpango wa muda mrefu ambao utajenga wastani wa nyumba 6,368 za magereza zitakazoweza kukaliwa na wastani wa kata 21,187. Bajeti ya fedha hizo zinahitajika zaidi ya shilingi trilioni 2.88 kwa ajili ya kukamilisha mradi huo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved