Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 79 2026-04-14

Name

Emmanuel John Khambay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. EMMANUEL J. KHAMBAY aliuliza: -

Je, lini Serikali itafanya maboresho ya makazi ya askari pamoja na kununua magari mapya Gereza la Babati Mjini?

Name

Mohammed Mahmoud Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Emmanuel John Khambay, Mbunge wa Babati Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Gereza la Babati ni miongoni mwa Magereza yaliyojengwa miaka mingi tangu mwaka 1974 hali iliyosababisha uchakavu wa miundombinu ya gereza pamoja na majengo ya makazi ya Askari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Jeshi la Magereza limeanza kutekeleza mpango mkakati wa muda mfupi na muda mrefu ambapo kwa Gereza Babati ziko nyumba tatu zinaendelea na ujenzi kwa kutumia mapato ya vyanzo vya ndani vya ubunifu. Aidha, katika mwaka wa fedha 2025/2026, Serikali imetenga shilingi 5,380,000,000/= kwa ajili ya ununuzi wa magari 31 kwa shughuli za Utawala na kusafirisha Mahabusu. Pindi magari hayo yatakapofika, Gereza la Babati litapatiwa gari moja mpya kwa matumizi ya kituo.