Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ali Vuai Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkwajuni

Primary Question

MHE. ALI VUAI KHAMIS aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga kituo cha Polisi katika Kijiji cha Matemwe Jimbo la Mkwajuni Unguja kutokana na uwekezaji mkubwa uliopo katika eneo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. ALI VUAI KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninapokea ushauri, pia nina maswali mawili ya nyongeza. La kwanza, Serikali ina mpango gani wa kuwapeleka askari wa doria katika eneo hilo ambalo liko mbali na kituo cha Polisi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, je, yuko tayari kutembelea Kijiji hicho kwenda kuona matatizo halisi ya umuhimu wa ujenzi wa kituo cha Polisi?

Name

Mohammed Mahmoud Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamshukuru sana Mheshimiwa Khamis kwa kufuatilia kwa karibu hali ya ulinzi na usalama katika Ukanda wa Mkwajuni hasa katika eneo la Matemwe, eneo ambalo ni ukanda wa utalii na lina ongezeko kubwa la idadi ya watu kwa sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, ninaomba kujibu hoja zake mbili. La kwanza, tuna mpango gani wa doria, kwa ukanda wote wa kuanzia Matemwe, Pwani Mchangani, Kiwengwa hadi Nungwi. Kwa sasa Jeshi letu la Polisi linaendelea na doria kwa sababu eneo lote hilo ni la kimkakati kwa ajili ya uwekezaji wa utalii, na kila siku Jeshi la Polisi kupitia Kituo Kikuu kilichopo Mkokotoni wanaendelea kufanya doria na Kituo Kidogo kilichopo Kiwengwa katika ukanda wote wa Pwani ambao amezungumza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa pili wa ombi lake la kutembelea hilo na kuona umuhimu wa kujenga kituo katika eneo hilo, napenda kukubaliana naye kimsingi kwamba eneo la ukanda wa Matemwe ni eneo la utalii, na kwa sababu ni eneo la utalii, kasi kubwa ya uwekezaji pamoja na ujio wa watalii na wageni mbalimbali kutembelea maeneo hayo, kunaakisi hoja aliyoileta ya kuweza kujengwa kituo katika eneo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo ninaomba nimjibu tu Mheshimiwa kwamba niko tayari kutembelea eneo hilo. Pili, tunaona umuhimu wa kujenga kituo cha Polisi katika eneo hilo.

Name

Jamal Ramadhan Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbwini

Primary Question

MHE. ALI VUAI KHAMIS aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga kituo cha Polisi katika Kijiji cha Matemwe Jimbo la Mkwajuni Unguja kutokana na uwekezaji mkubwa uliopo katika eneo hilo?

Supplementary Question 2

MHE. MWINYI JAMAL RAMADHAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa heshima hii ya kuuliza swali moja la nyongeza. Ninaomba kumwuliza Mheshimiwa Waziri, je, ni sababu zipi zinafanya kujengwa kwa kituo cha Polisi? Ni wingi wa watu, idadi ya uhalifu, kilometa, nyumba au ni nini?

Name

Mohammed Mahmoud Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nimemwelewa vizuri alichotaka hasa ni elimu ya kufahamu kwamba tunapokwenda kufanya maamuzi ya kujenga vituo vya Polisi, ni vigezo gani vinavyotusababisha kufanya maamuzi hayo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hivyo ndivyo, nataka kumwambia tu Mheshimiwa Mwinyi Jamal Ramadhan kwamba kwenye vyombo vya ulinzi na usalama kuna kitu kinaitwa security audit kwa maana ya ukaguzi wa kiusalama. Eneo ambalo linaonekana lina matishio zaidi ya kiusalama, ndilo eneo ambalo tunalipendekeza kuweza kuliwekea miundombinu ya kiulinzi vikiwemo vituo vya Polisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, wingi wa watu au idadi ya watu ni moja ya sababu, kasi ya ukuaji wa uchumi inaweza ikawa moja ya sababu, uhamiaji unaweza ukawa pia ni sehemu ya sababu.

Name

Asha Salum Motto

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALI VUAI KHAMIS aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga kituo cha Polisi katika Kijiji cha Matemwe Jimbo la Mkwajuni Unguja kutokana na uwekezaji mkubwa uliopo katika eneo hilo?

Supplementary Question 3

MHE. ASHA S. MOTTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza. Je, Serikali haioni haja ya kujenga nyumba za ghorofa kwa wafanyakazi wa Kituo cha Polisi Fuoni pamoja na kununua gari la doria?

Name

Mohammed Mahmoud Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Serikali inaona umuhimu wa kujenga nyumba za Polisi nchi nzima. Katika eneo la Fuoni hivi sasa zipo nyumba za Polisi, na baadhi yake ni za ghorofa, isipokuwa tu ninajua Mheshimiwa Asha amekuwa karibu na wananchi wake katika eneo la Fuoni na anafuatilia mwenendo wa hali ya usalama kwenye eneo lile na hasa kufuatilia ukamilishaji wa kituo cha Polisi pamoja na ujenzi wa nyumba za makazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa bahati, eneo hilo tumeshatembelea mimi na Mheshimiwa Asha, tumeshaliona na kubainisha baadhi ya maeneo yenye uhitaji wa kujengwa hizo nyumba na tayari tumetoa maelekezo kwa wenzetu wa Jeshi la Polisi kuweka mpango wa kujenga nyumba hizo kama ambavyo Mheshimiwa amependekeza.

Name

Mwamengo Ulimboka Baraka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. ALI VUAI KHAMIS aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga kituo cha Polisi katika Kijiji cha Matemwe Jimbo la Mkwajuni Unguja kutokana na uwekezaji mkubwa uliopo katika eneo hilo?

Supplementary Question 4

MHE. BARAKA A. U. MWAMENGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona na kunipa nafasi hii. Ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi cha Kasumulu kilichopo border ya Kasumulu ndani ya Jimbo la Kyela kwa kuwa kiliathirika na vurugu?

Name

Mohammed Mahmoud Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamshukuru sana Mheshimiwa Mbunge wa Kyela na nimpongeza vilevile kwa kuona umuhimu, na ninadhani kwa sababu ya ufafanuzi wangu wa hoja ya msingi ya kwa nini tunajenga vituo vya Polisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, narudi kwenye swali la msingi tulilojibu la Jeshi la Polisi kwa mara ya kwanza Bungeni, tulikuja na mpango wa dharura wa maeneo ambayo yana uhitaji wa kujenga vituo vya Polisi na tuliainisha wastani wa maeneo 698 nchi nzima. Hayo ndiyo maeneo ya dharura kujenga vituo vya Polisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maeneo hayo 698 ambazo ni karibu kata zaidi ya 600 zilikuwa hazina kabisa vituo vya Polisi na kata 77 zilikuwa zimeanza ujenzi kwa maboma, lakini hawajakamilisha. Nataka kumwambia tu Mheshimiwa kwamba tunaona umuhimu wa kujenga kituo cha Polisi eneo hilo, lakini lini? Mpango ule tumeugawa katika awamu tatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awamu ya kwanza tutakuwa na vituo 196, awamu ya pili tutakuwa na vituo 212 na awamu ya tatu tutakuwa na vituo 211. Kwa hiyo, kukamilika kwa Mpango huu, basi na eneo lake litakuwa tayari limeingia kwenye ujenzi.