Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 8 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 78 | 2026-04-14 |
Name
Ali Vuai Khamis
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mkwajuni
Primary Question
MHE. ALI VUAI KHAMIS aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga kituo cha Polisi katika Kijiji cha Matemwe Jimbo la Mkwajuni Unguja kutokana na uwekezaji mkubwa uliopo katika eneo hilo?
Name
Mohammed Mahmoud Ayoub
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Chaani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, kumjibu swali Mheshimiwa Ali Vuai Khamis, Mbunge wa Mkwajuni, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo la Matemwe Jimbo la Mkwajuni, hakuna sehemu iliyotengwa rasmi kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Polisi. Napenda kutumia fursa hii kupitia Bunge lako Tukufu, kumshauri Mheshimiwa Mbunge pamoja na Kamisheni ya Ardhi Zanzibar kupitia Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi ili kutenga eneo kwa ajili Kituo cha Polisi Matemwe, ili Serikali iweze kutenga fedha kutoka kwenye bajeti yake kwa ajili ya kujenga kituo hicho cha Polisi.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved