Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 78 2026-04-14

Name

Ali Vuai Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkwajuni

Primary Question

MHE. ALI VUAI KHAMIS aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga kituo cha Polisi katika Kijiji cha Matemwe Jimbo la Mkwajuni Unguja kutokana na uwekezaji mkubwa uliopo katika eneo hilo?

Name

Mohammed Mahmoud Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, kumjibu swali Mheshimiwa Ali Vuai Khamis, Mbunge wa Mkwajuni, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo la Matemwe Jimbo la Mkwajuni, hakuna sehemu iliyotengwa rasmi kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Polisi. Napenda kutumia fursa hii kupitia Bunge lako Tukufu, kumshauri Mheshimiwa Mbunge pamoja na Kamisheni ya Ardhi Zanzibar kupitia Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi ili kutenga eneo kwa ajili Kituo cha Polisi Matemwe, ili Serikali iweze kutenga fedha kutoka kwenye bajeti yake kwa ajili ya kujenga kituo hicho cha Polisi.