Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Ester Amos Bulaya
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ESTER A. BULAYA K.n.y. MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza kusafisha mafuta ghafi yanayotoka Uganda kupitia Bomba la Mafuta EACOP?
Supplementary Question 1
MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Mosi, je, katika mikataba iliyoingia Wizara ya Nishati, mmezingatia vipi maslahi ya nchi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kupitia mradi huo, Tanzania tutanufaika nini? Ahsante.
Name
Salome Wyckiffe Makamba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti ninakushukuru. Kwanza, ninampongeza dada yangu, Mheshimiwa Ester Bulaya kwa kufuatilia kwa karibu juu ya faida za Mradi huu wa Bomba la EACOP kwetu sisi Tanzania. Yako manufaa mengi ambayo Watanzania wameshayapata mpaka sasa hivi. Hivi tunavyozungumza, kipindi cha ujenzi wa bomba hili la mafuta, Watanzania zaidi ya 10,000 wamenufaika kwa ajira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo ya Mkoa wa Tanga ambako kimsingi ndiyo bomba hili linapoishia kwa ajili ya kutoa mafuta kupeleka nje, wananchi wale wamejengewa miradi ya maji, wamejengewa miradi ya barabara, wamechimbiwa visima na kama haitoshi, wamefanyiwa mafunzo mbalimbali kwa ajili ya upandaji wa miti na utunzaji wa mazingira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiachana na hilo, Tanzania itanufaika na uwepo wa bomba hili kwa sababu kuna asilimia ambayo nchi yetu itanufaika kama sehemu ya mradi wa bomba la mafuta. Ukiachana na hilo, sisi Watanzania tutapata faida ya kuuziwa sehemu ya mafuta hayo ghafi ambayo yakiwa yameshasafishwa tutayapata kwa ajili ya matumizi ya ndani ya nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, yako manufaa makubwa ambayo tunamshukuru Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kukubaliana na Mheshimiwa Rais wa Uganda, waliamua kufanya mradi huu wa kimapinduzi ambao unaenda kutatua changamoto ya mafuta na ya kiuchumi katika nchi yetu.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved